Posts

Showing posts from May, 2025

140. Tumsifu sisi Watu

1. Tumsifu sisi watu, tumsifu Mungu Baba, aliyeumba vyote kwa nguvu yake kuu. Wazima watu wote, na ndege wa angani wanyama wa mwituni, kwa huruma yake. 2. Tumsifu sisi watu, tumsifu Bwana Yesu, aliyetukomboa kwa damu yake tu. Amani tumepewa, hatuna hofu tena Ametuhurumia, Mwokozi ni yeye. 3. Tumsifu sisi watu, tumsifu Roho, ndiye Mtulizaji popote, furaha iwe kuu. Moyo umetulia, amani umepata, wamwombao yeye.

141. Tumpeni Sifa na Tukuzo

Tumpeni sifa na tukuzo, sifa na tukuzo ni zake, Ukuu na nguvu zote zimpasaye Mungu, ni vya Bwana, ni vya Bwana  na vimtii siku zote. Tumpeni sifa na tukuzo,  sifa na tukuzo ni zake.  Sifa, maombi na  nguvu zote ni za Bwana  siku zote, kale yote  hata itakayokuja.  Amen. Amen. 

142. Vyenye Uzima Vimtukuze

Vyenye uzima vimtukuze, vimtukuze Bwana,  vimtukuze, vimtukuze,  vimtukuze,  hata na utakatifu wake.  Kwani ameumba mbingu  na nchi.  Vyenye uzima vimtukuze,  vimtukuze Bwana,  vimtukuze Bwana,  vimtukuze Bwana, vimtukuze Bwana.  Na magunda na mazeze  na filimbi na vilangwi  na vinanda  na vimtukuze!  Vyenye uzima na viimbe,  vimtukuze Bwana!  Na magunda na vinanda  Vyote vimtukuze  ee Bwana wa majeshi!  Haleluya!

143. Utukufu ni wa Mungu

Utukufu ni wa Mungu juu,  tukuzo lote, uwezo wote ni wa  Mungu, Bwana wetu, Bwana wetu,  Mungu ni wa pekee  Shangilio lake lijaze katika dunia  popote,  Jina lake litukuzwe na watu wote. Tumshangilie Mungu wetu  na Bwana wetu  nyimbo za tukuzo  Tumpeni heshima zote,  tumwimbie,  Sifa na tukuzo zampasa,  zote ni zake Mungu wetu! 

144. Bwana, Bwana Ndiye Mtakatifu

Bwana, Bwana ndiye  mtakatifu,  anayo nguvu na sasa aliyeko,  na ajaye,  Bwana! Bwana! Mungu,  Mfalme, mwenye uwezo!

145. Bwana Wema Wako Popote

Bwana wema wako popote  hata mbinguni huko juu. Bwana  wema wako popote hata  mbinguni huko juu.     /: Na welekevu, na         welekevu/: wako huenea na  mawinguni  na walekevu wako  huenea na mawinguni.       /:Haleluya x 4       Haleluya x 2/: 

146. Mwenyezi, Mwenyezi, Mwenyezi

Mwenyezi, Mwenyezi, Mwenyezi,  Jina lako litukuzwe sana.  Amin, Amin.  Hata ulimwengu wetu uteketezwe kwa moto.  Nazo nyumba zetu,  ziimbe utakatifu wake,  Haleluya, Haleluya.

147. Mtakatifu Wewe, Mungu

1. Mtakatifu Wewe,    Mungu Mwenye enzi,     jua likitoka tutakutukuza wee.    Mtakatifu Wewe     wa huruma nyingi,    Mwenyezi Mungu wa Utatu. 2. Mtakatifu Wewe,     waliookoka wakusujudia Wewe     huko daima.    Makerubi wote wakuinamia,    Mwenyezi Mungu wa Utatu. 3. Mtakatifu Wewe, siri wajificha,     macho yetu     hayawezi kukutazama,     Wewe peke yako     Mtakatifu kweli,     Mwenyezi Mungu wa Utatu. 4. Mtakatifu Wewe    Mungu Mwenye enzi,     kazi zako zakusifu kila mahali.     Mtakatifu Wewe     wa huruma nyingi,     Mwenyezi Mungu wa Utatu.    Amen. 

148. Mungu Baba, Mungu Mwana

1.  W:  Mungu Baba, Mungu         Mwana, Mungu Roho,          twakusifu twakushangilia          sote, Umejifunua kwetu          kwa upendo,          kwamba wanadamu          wakujue wote.      K:   /: Mungu wetu      W:  Anapenda tuwe wake     K:  Dhambi zetu     W:  Tuache, tumfuate.:/ 2.  W:  Mungu Baba wewe          uliumba vyote, Mbingu,           dunia na vilivyomo vyote,           watu, ndege na          wanyama uliumba,           Jua, mwezi  na nyota           vyakutukuza.     K:  /: Mungu wetu:/ 3.  W:  Mungu Mwana,       ...

149. Chini ya Bawa Lako

1. Chini ya bawa lako,     ee Yesu nifiche    Unipe raha kwako    kwenye mambo yote.     Na uwe yote kwangu,     hekima, shauri,    na siku zangu zote     niwe na amani. 2. Nisamehe makosa     nioshe kwa damu,     unipe nia safi    na mapenzi mapya.    Wakubwa na wadogo     ututunze sote,    na kwa amani yako     tupate furaha.

150. Ahimidiwe Mwamba Wangu

1. Ahimidiwe mwamba wangu,    ahimidiwe ngome yangu, wema     wake wapita vyote duniani. 2. Aturuzuku kila kitu,    atugawia mema kwetu     wema wake wapita vyote    duniani. 3. Upendo wake mwingi sana,    katutolea Mwana wake, wema    wake wapita vyote duniani. 4. Katika Yesu, Mwana  wake,    Twapatanishwa naye  Baba,    wema wake wapita vyote     duniani. 5. Ashukuriwe Mungu wetu,    sifa zote ni zake Bwana    wema wake wapita vyote    duniani.

151. Ee Moyo Wangu, Hima

1.  Ee moyo wangu, hima,     enenda mbinguni!      Ulimwenguni humu      hapana pa raha.     Mchungaji wetu Yesu     achungapo kondoo     ni penye raha kuu.      Enenda mbinguni! 2. Yeye akupokee,     Mungu Baba yako,     akuketishe pake     katika enzi kuu.    Atakuvika nguo    za wongofu wa Mungu,     akupa raha kuu.    Enenda mbinguni! 3. Nakutamani sana    Mwana Kondoo Mungu!     Ningepata mabawa     ningeruka pale,    wanaposhangilia     malaika wake Mungu     katika raha kuu.     Enenda mbinguni! 4. Mapenzi yako Bwana     ndizo haja zangu,     Utakalo lolote    nami nitatenda.    Naingojea siku     utakayoniita,     nipate raha kuu!...

152. Mahali pa Raha

1. Mahali pa raha ya moyo wapi?     Akukingiaye mabaya nani?    Dunia haina makimbilio,    nisiposhindwa na makosa yangu.        /:Sipo, sipo hapa sipo,           mbinguni ni ngome          ya moyo wangu. :/ 2. Iache dunia, uone ngome,     unapofurahishwa moyo wangu.    Ni Yerusalemu unaojengwa    na mawe mazuri ya dhahabu tu.         /: Ndiko, ndiko,             ndiko ngome            na makimbilio            ya moyo wangu. :/    3. Mwangani kwa Yesu     ni raha tamu,    hakuna makosa na shida huko.    Vinubi na sauti za nyimbo nzuri    zinaufurahisha moyo huko.           /: Raha, raha, raha tamu             mbinguni ...

153. Ninapenda Kwenda Zangu

1.  Ninapenda kwenda zangu     nimwone Mwokozi      wangu.     Moyo wangu watamani     kuambatana na Yesu           /: na kumsifu milele. :/ 2.  Ninapenda kusikia      nyimbo za malaika wote.     Ningekuwa na mabawa      ningeruka leo hivi           /: mpaka Sayuni                kwake.:/ 3.  Ninapenda kuingia     pale penye utukufu,     penye nyumba za dhahabu     nimwone Mwokozi      wangu           /: na furaha za mbingu:/ 4.  Ninapenda kuuona      uzuri wa Paradiso.     Nikifika nitapata      tunda lake tamu sana,         /: Yesu, nipeleke juu! :/

154. Ninataka Kuingia

1. Ninataka kuingia     mjini kwa Mungu.     Nitashinda, nitakaza     mwendo nifike,     nikishikwa na shida,    nikichoka njiani,     Yesu unaniambia:     “Uningojee!” 2. Naitwa na Yesu Kristo    enzini mwake.    Nakimbia, kukawia     hakuna faida,    wote wachelewao     hawatapata taji.     Mimi sitaki kingine     ila uzima. 3. Elekeza macho yangu    mlangoni pako.     Niongoze, nipe nguvu,     ninapochoka.     Ninapojaribiwa,     ninaposingiziwa,    Yesu, unisaidie     nisikuache. 4. Mkono wako     unishike nisianguke.    Najiona kuwa mnyonge,    nguvu i kwako,    Neno lako, ee Yesu,     linanipa uzima.     Nikifika, nitaimba, ...

155. Ondokeni! Tunaitwa

1. Ondokeni! tunaitwa     na walinzi wa juu     mnarani     Yerusalemu, amka wee!     Ni usiku wa manane,    yuaja Bwana wa arusi,     wanawali wako wapi?     Amkeni upesi!     Kaziwasheni taa.     Haleluya!    Fuateni arusini     kwenda kumpokea     Bwana! 2. Sayuni anasikia,     moyo waruka kwa furaha,     yu macho anaondoka.    Mponya wake anashuka     mbinguni mwenye     utukufu,     aleta mwanga wa kweli,     taji yake yaja    na Mwana wa Mungu.     Hosiana!    Twafuata kwenye shangwe     tukale karamu yake. 3. Waimbiwa nyimbo nzuri     kwa misemo ya watu wote     na ya malaika mbinguni.    Tukifika mjini kwako    kwen...

156. Umejengwa Juu Yerusalemu

1. Umejengwa juu Yerusalemu,    ninakutamani.    Moyo wangu ukikutamani,     wataka kupita milima na    mabonde, kuruka kama tai,     uache ulimwengu     uingie kwako.  2. Siku nzuri! Ninaingojea,     ifike upesi.    Niiache dunia niende     mbinguni kwa shangwe.    Nimrudishie roho     Mwokozi Bwanangu,     aipokee vema, aipe uzima. 3. Mara moja roho itakwenda    kufika mbinguni,    ikiacha uzima wa hapa     kwa nguvu ya Mungu.    Yapelekwa na gari     kama Eliya mkuu,     malaika waibeba     vizuri kwa shangwe. 4. Nikifika kule Paradiso, mwisho    huu ni mwema.     Roho yangu yajaa furaha,    kinywa husifu tu.    Wateule huimba     nyimbo nzuri nyingi,     hawaachi ...

157. Mjini ni Mbinguni

1. Mjini ni mbinguni kwa Mungu,    hakuna mabaya na shida,    waongofu wengi wamejaa    wanaomsifu Mwana Kondoo         Mbinguni, mbinguni         mjini ni mbinguni         kwa Mungu.          Mbinguni mbinguni          kwa Mungu ndio mji wa         kutupendeza. 2. Wateule wengi wa huko    wanaoangazwa na Yesu,    huko kuna furaha yetu.     Jua lake ni la uzima.          Mbinguni, … 3. Moyo wangu una furaha     ya kwenda mbinguni kwa     Mungu. Bwana univute uliko,    kiaga chako kitimie!             Mbinguni, …  4. Kitambo kidogo kipite    na mimi nifike mbinguni.    Bwana wangu Yesu nakuomba:    Ukoo wangu wote ufike    ...

158. Liko Pumziko la Mioyo

1.  Liko pumziko la mioyo,      amka wee unayechoka,      Unaugua kama mfungwa kwa     shida za moyo wako      Umtazame Kondoo wa Mungu      atakuchunga kwa furaha.     Uache mzigo enenda.      Vita nzuri yamalizika,     safari yabaki kidogo      inayokusumbua mno. 2.  Mungu ametuchagulia      pumziko lisilo mwisho     Amelitengeneza kale,      mtu hajazaliwa bado,      kufa kwamfurahisha  Mponya,     tupate pa kupumzikia.      Aita, anaalika      mioyo inayokaa na shida,      msikawie, njooni leo!     Ingieni pumzikoni! 3.  Ninyi mshindwao na mizigo     mlemewao na uzito      Rukeni kimbieni hima,      tokeni pangoni mwenu;     msienende kwa kuinama,     Mponya anawaambie...

159. Mbinguni, Mbinguni

1. Mbinguni, mbinguni     kuna mji mwema.          /: Wapendeza sana,           ni wake Mungu. :/ 2. Milango ya mjini  ni dhahabu tu,         /: Mungu ndiye jua             anaung’aza. :/ 3. Ugonjwa hauko, kufa hakuna.         /: Wenyeji wa humo ni               wa kweli tu :/ 4. Waimba usiku hata na mchana         /: Wakimsifu Bwana            Mungu wetu tu. :/ 5. Wote waimbao wana furaha.         /: Wang’azwa na damu              ya Bwana Yesu. :/ 6. Vijana sikieni wote kwamba.        /:Twapendwa na Yesu,            Bwana wa mbingu. :/ 7. Twendeni kuingia wote mjini,          /: Tupewe uzima na ...

160. Maisha ya Duniani

1. Maisha ya duniani ni mafupi,    hata siku ni chache;     zinapita hima na kutoweka    wala hazirudi, zinatokomea. 2. Vivi hivi kila mmoja     tunakwenda     mbinguni kwake Mungu,    mbele ya kiti chake     cha hukumu    kila mtu atapewa haki yake. 3. Tunakwenda huko sote    na waamini    waamini waenda bila woga    kwani wanaye Bwana     wanaiingia nchi takatifu. 4. Ee ndugu, twendeni sote    kwake Mungu.     Ulimwengu wapita;     utaangamia na dhambi zako,    usipokubali nawe waangamia. 5. Basi ndugu tujikabidhi     kwa Mungu tuwapo bado hai;    kwani tukipuuza tutapotea,     hatutaepuka hukumu milele. 

161. Watumwa wa Yesu

1. Watumwa wa Yesu jitayarisheni,    shikeni Neno la Yesu     kesha kila siku. 2. Tengenezeni taa, wekeni mafuta,    jifungeni muwe mbele,     hata kukimbia. 3. Omba usikome ninakuja sasa,    angalia nawaonya,     hima njooni kwangu. 4. We utaokoka, ukikaa kwake,    kutazama uso wake     utavikwa taji. 5. Bwana huandaa wateule wake,     awachukue mbinguni,     karamuni mwake. 

162. Bwana, Twakuletea

1.  Bwana, twakuletea     mtoto huyu, (watu hawa)      tukijua amri yako ya mwisho      uliyowapa mitume:      Watu wote wabatizwe,     watakaokuwa wako.   2. Neno hili ni kubwa     tulilopewa na Yesu:     Atakaye kufika katika ufalme     wako,      hana budi kuzaliwa    tena kwa maji na Roho. 3. Pokea kondoo wako    Mchunga mwema Bwana Yesu    Umwongoze mbinguni     (Waongoze mbinguni)     ndiwe njia na uzima.     Umpe kukutegemea     (wape kukutegemea)     apate kutengemana     (wapate kutengemana). 4. Baba, tunakusihi    ukubali wimbo wetu,     usikie maombi     tunayokuomba sasa.    Andika jina la mtoto     (Andika majina yao)     katika kitabu chak...

163. Mungu Upokee Moyo Wangu

1. Mungu upokee     moyo wangu wote,    niwe mtoto wako,     siku zangu zote.    Nikufuate Wewe     nisikuache tena,     nishike siku zote,     ulivyotuagiza.    Unisaidie mimi,     hata kufa kwangu. 2. Msalabani pako,     Yesu naanguka,     uliyenifia    hata mimi pia.    Yaondoe makosa     yatoweke kabisa,     nipate kuwa safi     kwa damu yako bora.    Unisaidie mimi     hata kufa kwangu. 3. Roho Mtakatifu,     unanipa nguvu;    niweze kushinda     majaribu yote,     naomba: utawale     katika moyo wangu,    Shetani, hata kufa,     asinishinde mimi.    Unisaidie mimi,    hata kufa kwangu. 4. Baba, Mwana, Roho     uliye m...

164. Tumekujia Bwana Wetu

1. Tumekujia Bwana wetu     kujiweka mkononi mwako,    tuwe wako hata milele    twakushukuru na twakusifu.    Mwokozi wetu, utukubali,     utuongoze njia ya mbingu. 2. Twataka kubatizwa leo     kwa Jina lako, tuwe Wakristo.    Umetukomboa na sisi     ulipokufa pale Golgota,     na kwamba wewe upo karibu,    unasikia kuomba kwetu. 3. Twakupambia mioyo leo,     ingia, Mfalme wa utukufu!    Utupe sisi nuru yako    tuwe mwanga katika dunia.    Pokea leo mioyo yetu,     tunajitoa kwako wenyewe. 4. Tunakuomba sasa, Bwana,    usitutie majaribuni.     Utuongoze siku zote,     tukufuate wenye imani.    Mwisho tufike kwenye enzi kuu,    tuipokee taji ya mbingu.

165. Mimi ni Mtoto Mdogo Tu

1.  Mimi ni mtoto mdogo tu      na nguvu sinayo.     Nataka kwenda mbinguni     na njia sijui. 2.  Nitapotea kabisa      katika makosa.      Usiponisaidia      Mwokozi ee Yesu. 3.  Ulikuwa mtoto mdogo      kwa ajili yangu.     Nakupa moyo wangu      huu, uwe mali yako. 4.  Naomba utangulie,      nishike mkononi!      Mimi nitakufuata,      tufike nyumbani.

166. Wamwendea Yesu

1. Wamwendea Yesu    kwa kusafishwa,    na kuoshwa     kwa damu ya Kondoo?     Je neema yake umemwagiwa?     Umeoshwa     kwa damu ya Kondoo?         Kuoshwa, kwa damu           itutakasayo ya Kondoo;         Ziwe safi nguo nyeupe           mno: Umeoshwa         kwa damu ya Kondoo? 2. Wamwandama daima     Mkombozi na kuoshwa     kwa damu ya Kondoo?     Je, waishi kwake msulibiwa?    Umeoshwa     kwa damu ya Kondoo?          Kuoshwa … 3. Atakapokuja Bwana arusi     uwe safi kwa damu ya kondoo.    Yafae kwenda Mbinguni mavazi    yafuliwe kwa damu ya kondoo.             Kuoshwa … 4. Yatupwe yaliyo na takataka,  ...

167. Ni Siku Kuu Siku Ile

1.  Ni sikukuu siku ile      ya kumkiri Mwokozi!      Moyo umejaa tele,     kunyamaza hauwezi.            Siku kuu! Siku kuu!             ya kuoshwa dhambi              zangu kuu.            Hukesha na            kuomba tu,            ananiongoza miguu.            Siku kuu! Siku kuu!            Ya kuoshwa dhambi            zangu kuu. 2.  Tumekwisha kupatana     mimi wake, Yeye wangu,      na sasa nitamwandama,      nikiri Neno la Mungu.             Siku kuu! … 3.  Moyo tulia kwa Bwana      kiini cha raha yako, huna njia     mbili tena:      Yesu...

168. Shika Mikono Yangu

1. Shika mikono yangu, niongoze,    mpaka nimalizapo safari hii.    Nikiwa peke yangu napotea.    Popote uendapo nipeleke! 2. Tuliza moyo wangu, uwe kimya,    nikiona furaha au majonzi,    unitulize sana, ndimi wako,    sitaki neno tena, ila hilo. 3. Nisipoona leo nguvu yako,    najua wanilinda, huniachi.    Shika mikono yangu niongoze,    mpaka nimalizapo safari hii! 

169. Rafiki Bora Yu Mbinguni

1. Rafiki bora yu mbinguni,    duniani rafiki haba,     sababu hapa mapatano     yanavunjika upesi.         Kwa hiyo mimi nasema:         Rafiki bora ni Yesu. 2. Dunia ni kama utete!    Yesu ni Mwamba wa nguvu.    Ningeachwa na watu wote,    Yeye haniachi kamwe.           Kwa hiyo … 3. Maisha yake ametoa,     nami ninajitoa kwake.    Anipenda bila kuchoka,     ashinda hata kaburi.           Kwa hiyo …

170. Yesu Wangu Simwachi

1. Yesu wangu simwachi,    kwani amenikomboa.     Akitoa maisha,     kulipa madeni yangu.            Sasa namwelekea,             Yesu wangu simwachi! 2. Yesu wangu simwachi,    siku zote za duniani.     Nimempa yangu yote,      ayashike mikononi.              Sasa namwelekea..... 3. Yesu wangu simwachi,    anichunga kwa upole     malishoni vizuri,     mwenye shangwe ampendaye:              Sasa namwelekea.....

171. Nimepita Ulimwengu

1. Nimepita ulimwengu,    ulimwengu ni mzuri,    lakini natamani     ulimwengu mwingine. 2. Nimeona watu wengi,    hutafuta daima,    Maisha yao yote,     ndiyo taabu na shida.  3. Imebaki hali njema     ya furaha ya roho:     Hubirini pote pote;     taabu itatulia. 4. Msalabani pa Golgota     jerahani mwa Yesu     ni mahali penye raha     kwao wote kabisa. 

172. Nitwae Hivi Nilivyo

1. Nitwae hivi nilivyo,     umemwaga damu yako,     nawe ulivyoniita,          Bwana Yesu, naja, naja. 2. Hivi nilivyo si langu    kujiosha roho yangu.    Nisamehe dhambi zangu,          Bwana Yesu, naja, naja. 3. Hivi nilivyo sioni     kamwe furaha moyoni.    Daima ni mashakani,           Bwana Yesu, naja, naja. 4. Hivi nilivyo kipofu,     maskini na mpungufu.     Wewe u mtimilifu;          Bwana Yesu, naja, naja. 5. Nawe hivi utanitwaa,     nisithubutu kukawa,     na wewe hutanikataa.           Bwana Yesu, naja, naja. 6. Hivi nilivyo mapenzi yamenipa    njia wazi, hali na mali sisazi,            Bwana Yesu, naja, naja.  

173. Yesu Mkononi Mwako

1. Yesu mkononi mwako     nitalindwa vema.    Raha bora napata    kwa upendo wako.    Nawe kwa sauti tamu     waniita mimi:    Wacha tu nguvu yako,     kwangu ni raha kuu.     Yesu mkononi mwako     nitalindwa vema,     raha bora napata     kwa upendo wako! 2. Yesu mkononi mwako     sioni taabu.    Shetani nguvu zake    haziwezi kwako.    Shaka na woga kwako     zinakosa nguvu,     na majaribu yote     nayashinda pia.          Yesu mkononi … 3. Umenifia Bwana,     nakukimbilia.     Wanishika milele,     nakutegemea.     Nakungojea hapa     na giza liishe,     mchana wapambazuka     na kwako milele.     Yesu mkonon...

174. Ewe Baba, Bwana wangu

1. Ewe Baba, Bwana wangu,    nielekeze mwenendo     nifuate Neno lako     hata leo kaa kwangu!     Uwe mlinzi na ngao    uongoze maisha mpaka nifike    kwako! 2. Umenipa na wazazi     walio mkono wako,    wanifundisha vizuri,     hata na wadhamini,     walimu na wakuu     Baba Mungu naomba     nao uwaongoze! 3. Hata ndugu zangu wote     umenipa kwa wema,     nisaidiane nao     siku zote kwa pendo.    Utupe kuungana    wakubwa tuheshimu     kwa maneno mazuri! 4. Ulikuze kundi letu     tukae na adabu,     tuinue nchi yetu     siku zitungojazo!    Nao ufalme wako     uenezwe na kwetu,    uheshimiwe! Amen.

175. Heri Kumjua Yesu, Bwana

1. Heri kumjua Yesu, Bwana.    Roho huamka, aniita.    Anitambua mali yake,     hanipotezi,  niko kwake.           Msimuliwe sifa zake:            Hana mwenzake,             Mponya pekee,              afurahisha moyo kweli.            Yeye ni Yesu,               tumtukuze. 2. Nikimwambia mambo yote    anituliza moyo vema.     Nikimfanyia kazi zangu,     anibariki hapa na juu.            Msimuliwe … 3. Nikimjutia nimekosa,     anaondoa na mashaka.     Yeye hapendi nikishindwa,    anipa nguvu za kwendea.             Msimuliwe … 

176. Tumiminie ee Mtakatifu

1. Tumiminie ee Mtakatifu,     Roho wako mwenye nguvu    atakase mioyo yetu,     tuwe wako tu kale na kale! 2. Wewe mwenyewe,     tulinganishe    tuungame kwa furaha,    ya kuwa u Bwana wetu,    tena Mwokozi    kwa damu yako! 3. Tukutazame     kwa mioyo yote,    tukilirudisha upya     agano la ubatizo,    tukufuate, tuache yetu! 4. Tukija sasa kubarikiwa,    sikia kuomba kwetu,     tugawie mema mengi,     tutengemane     mwangani mwako! 5. Na atujie Roho wa Bwana,    atuunganishe sote     kuwa kundi takatifu     mpaka tumwone     kwake mbinguni! 

177. Nitakase, Unishike

1. Nitakase, unishike,    nifunike, unilaze! 2. Nipe kuwa mpole, mwema!    Tupatane sikuachi. 3. Niwe wako peke yako!    Nakuita, nakupenda. 4. Uliteswa, ulikufa;    wanifia mimi mwovu. 5. Ulitaka kutuponya,     kutufanya watu wapya!  6. Wewe pekee Mponya wangu;    mkono wako unishike!

178. Neema ya Bwana Yesu Kristo

Neema ya Bwana Yesu Kristo, na upendo wa Mungu, na ushirika wa Roho Mtakata,  ukae nasi, sisi sote, Amen.

179. Yesu Kwa Imani

1. Yesu kwa imani, nakutumaini,     peke yako.     Nisikie sasa na kunitakasa,    ni wako kabisa tangu leo. 2. Nipe nguvu pia za kusaidia    moyo wangu.    Ulikufa Wewe, wokovu nipewe,    nakupenda Wewe,     Bwana wangu. 3. Hapa nazunguka     katika mashaka, na matata.     Palipo na giza utaniongoza     hivi nitaweza kufuata. 4. Takuwa mzima    nivushe salama mautini.     Sina hofu kamwe     ukiwapo nami,     nami nikwandame siku zote.

180. Bwana, u sehemu yangu

1. Bwana, u sehemu yangu,    Rafiki yangu, Wewe;     katika safari yangu     nitembee na Wewe.          Pamoja na Wewe,           pamoja na Wewe,           katika safari yangu           nitembee na Wewe. 2. Mali hapa sikutaka     ili niheshimiwe,     heri nikute mateso     sawasawa na Wewe.          Pamoja na Wewe,           pamoja na Wewe,            heri nikute mateso           sawasawa na wewe. 3. Niongoze safarini,    mbele  unichukue.     Mlangoni mwa mbinguni     niingie na Wewe.            Pamoja na Wewe,             pamoja na Wewe,      ...

181. Enyi Wakristo, Kumbukeni

1. Enyi Wakristo, kumbukeni hivi:    Sisi tunaokula mkate mmoja     tunaokunywa kinywaji kimoja,     tu mwili mmoja. 2. Tukipatana vema kama ndugu,    tukiwasaidia  wenye shida,    tukiwashika walio wanyonge     twamtii Bwana. 3. Tukikumbuka     pendo lake kubwa,    tutapendana nasi mpaka kufa.    Ee, Bwana, utimize shauri hili    vizuri kwetu.

182. Nuru ya Rohoni

1. Nuru ya rohoni ni Bwana Yesu.    Nakuomba sana niangazishe;     ukanitazame kwa huruma tu,         /: Ukanitulize             mimi maskini. :/ 2. Futa dhambi zangu     kwa damu yako.     Hasira ya Mungu iniondoke.     Machubuko yako, hata mateso,        /: Niyawaze vema           rohoni mwangu. :/  3. Nakutumaini peke yako tu,    niwe mtumwa wako     pote nilipo, utanikubali,     sina mashaka!         /: Nitakushukuru          pasipo mwisho. :/

183. Usiku Ulipotolewa

1. Usiku ulipotolewa,    Yesu, umetugawia     mapato ya mateso yako,    tukumbuke kufa kwako.    Waaminio wakusifu     wakija karamuni kwako. 2. Tunakumbuka kufa kwako,    tukila  mwili wako huu;     twapewa nguvu ya uzima     tukinywa damu yako hii.    Karamu hii tunayopewa     yatuonyesha pendo lako. 3. Huu mkate ni chakula kweli,    hii damu yatutuliza;    mioyo yetu yapumzishwa     tukila mezani kwako.     Tunaongezwa nguvu zetu,     za kukutegemea vema. 4. Twashirikiana na wote    walio viungo vyako;     kwani tunashibishwa sote     kwa mwili na damu moja,     tu kundi la Mchungaji mmoja;     kwa hivi twapatana sote. 5. Twapewa mwili wako Bwana,    tujue kweli ya kwamba     miili yetu ya unyonge...

184. Moyo Wangu Ujipambe

1.  Moyo wangu ujipambe,     acha mambo ya gizani.      Kaza mwendo wa nuruni      hivi utang’aa vizuri.      Kwani Bwana wa rehema      akukaribisha kwake.      Mwenye utukufu mwingi     anapenda kuja kwako. 2.  Amka ukamlaki yeye,      umkaribishe vizuri.     Abishaye hodi kwako,      akuleteaye neema.     Umkubali kwa furaha      aingiaye moyoni.     Sema: Bwana, nakupenda,      sikuachi siku zote. 3.  Hatuwezi kufahamu      mambo haya ya ajabu:     Unapenda kuwa nasi      kwa mkate na kwa mvinyo.     Yesu, tunaomba sana:      Wewe kaa leo hapa,      tugawie neema yako,      Chakula Kitakatifu. 4.  Yesu, jua la rehema,     Yesu,chemchem ya uzima,     Yesu, nakupenda san...

185. Bwana Wetu Ametoa

1. Bwana wetu ametoa     mara moja msalabani     mwili na maisha yake    kwa wokovu mkamilifu. 2. Ndiye kafara ya kweli    itoshayo siku zote;    kima chake ni kikubwa    hakiwezi kuzidishwa. 3. Mbinguni atuombea     akiwa kitini pake.    Na hapa atubariki,    tukila karamu yake. 4. Twaonyesha kufa kwake    mpaka atakaporudi;     tunaungana na Yeye     kuwa viungo vyake tu.

186. Mfalme wa Upendo Ndiye

1. Mfalme wa upendo ndiye     anichungaye mimi,    Yeye ni wangu milele,    ananipenda daima. 2. Kwenye maji ya uzima     hunipeleka mimi    katika malisho mema,     anilisha siku zote. 3. Mara nyingi napotea    kwa ukaidi wangu,     naye ananitafuta,     na kunirudisha kwake. 4. Kivuli cha kufa kwangu     sitaogopa tena,    ukiwa kwangu daima     mashaka wayaondoa. 5. Wanitandikia meza,     naula mkate wako,     nanywa katika kikombe    nikumbuke kufa kwako.  6. Siku zangu zote hapa      wema wako u vivyo.    Nikubali Mchunga mwema,    nikuimbie milele.

187. Kama Ulivyoagiza

1.  Kama ulivyoagiza      kabla kuuawa,      hivi nitafanya, Bwana      nitakukumbuka. 2.  Wewe kwa ajili yangu      ulitoa mwili     katika mkate wako huu,     nitaukumbuka. 3.  Vivyo damu ya thamani     Wewe ulitoa.     Katika kikombe hiki,      nitaikumbuka. 4.  Nitazamapo Golgota,     kuona msalaba,     na kipaji cha kafara      nitakikumbuka. 5.  Siwezi kusahau  jinsi      ulivyoumia,     kweli nikiwapo mzima      nitakukumbuka. 6.  Kwa hiyo nakungojea      Ee Bwana kwa kuwa     ujapo mara ya pili      utanikumbuka.

188. Sioshwi Dhambi Zangu

1.  Sioshwi dhambi zangu,     bila damu yake Yesu.     Hapendezewi Mungu,      bila damu yake Yesu.          Hakuna kabisa            dawa ya makosa           ya kututakasa,           ila damu yake Yesu. 2.  La kunisafi sina,      ila damu yake Yesu.     Wala udhuru tena,      ila damu yake Yesu.          Hakuna kabisa … 3.  Sipati patanishwa,      bila damu yake Yesu.     Hukumu yanitisha,      bila damu yake Yesu.           Hakuna kabisa … 4.  Sipati tumaini,     bila damu yake Yesu.      Wema wala amani,      bila damu yake Yesu.           Hakuna kabisa … 5.  Yashinda ulimwengu,      hiyo da...

189. Uuchunguze Ndani Yangu

1.  Uchunguze ndani yangu,      iwe safi nia,     kwangu kama kwako     Mungu, idhihiri pia. 2.  Uchunguze moyo wangu      unifunulie,      yaliyomo ndani yangu,      nami niyajue. 3.  Kwanza washa zako tambi,     kumefunga giza,     nijue ambavyo dhambi     ni ya kuchukiza. 4.  Uchunguze na mawazo,     ni mbegu za mambo.      Asili ya machukizo,      maumbuo umbo. 5.  Uzidi kuyachunguza     katikati yangu.     Hata uishe nifundisha      udhaifu wangu.  6.  Hapo nikikuinamia      mbele zako Mungu,     hakika nitakujua      ndiwe mpenzi wangu.

190. Onjeni, Onjeni

1.  K:  Onjeni, onjeni.      W:  Onjeni, muone kuwa          Bwana ni mwema,           onjeni.      K:  Heri.     W:  Anayemtumaini,      K:  Heri      W:  Anayemtumaini,           ni heri   2.  K:  Mcheni, mcheni.     W:  Mcheni Bwana,           mlio watakatifu,           mcheni.      K:  Wale      W:  Wanaomcha Bwana.      K:  Wale      W:  Wanaomcha Bwana           ni heri.   3.  K:  Na simba, na simba.     W:  Na simba hutindikiwa,          Huona njaa, na simba.     K:  Bali      W:  Wamtafutao Bwana,  ...

191. Njooni Tule Karamani

1.  K:  Njooni tule karamuni.     W:  Njooni tule karamuni.       K:  Huu mkate mwili          wake Yesu.     W:  Huu mkate mwili wake           Yesu 2.  K:  Njooni, tunywe           karamuni.      W:  Njooni, tunywe           karamuni.     K:  Huu mvinyo damu yake         Yesu      W:  Huu mvinyo damu yake          Yesu. 3.  K:  Yesu yu pamoja nasi.     W:  Yesu yu pamoja nasi.      K:  Tumekutanika naye         Bwana     W:  Tumekutanika naye          Bwana 4.  K:  Jipe moyo, ndugu           yangu,     W:  Jipe moyo, ndugu     ...

192. Nyumba Hubarikiwa

1.  Nyumba hubarikiwa ukaamo,     Yesu, uliye mpenzi wa mioyo,     wakukaribishapo kwa furaha,     uliye mgeni wa heshima kuu.     Mioyo yetu inapokupenda      na macho yote yakungojapo,     midomo yote ikuulizapo,     na watu wote wanapokutii. 2.  Nyumba hubarikiwa,      mume na mke      wanapopatana kukupenda.     Wakikumbuka, kama wamepewa      wokovu mmoja nawe, ee Yesu.     Wakushikapo na kutegemea,     wakati wa furaha na shida,     wasipoacha njia ya uzima hata     huzuni ikiwashika. 3.  Nyumba hubarikiwa,      wawekwamo     watoto wakujue, wakutii.     Uwapendaye na kuwabariki     watoto walio kondoo wako.     Wanapokusanyika wa nyumbani,     wasikilize Neno lako tu,     wanaposhirikiana kuomba      na kukufu...

193. Ndoa Yetu Nzima

1.  Ndoa yetu nzima simika, Yesu!     Usiku na mchana uwepo kwetu.     Leo tuna raha, Wewe watupa.         /: Ndoa yetu Bwana            ndiwe baraka!/: 2.  Atoka kijana, ataka mchumba     siku zinapita  za kupimana.     Leo twapatana pamoja kukaa          /: Ndoa yetu … /: 3.  Vyote hapa chini vinakaa muda,     vyote vinaoza, tena vyachakaa.      Pendo la dunia nalo huchakaa.           /: Ndoa yetu … /:  4.  Kaa kwetu Bwana, kutukagua,     pendo letu sisi lisichakae:      Hivi natukae na baraka tu.            /: Ndoa yetu … /: 5.  Kana arusini ulialikwa,      walivyoishiwa ukaongeza,      nasi shida zetu utazishinda.            /: Ndoa yetu … /:

194. Yesu Nitakuimbia

1.  Yesu nitakuimbia     kwa rehema zako zote.     Baraka nyingi sana      nimepata kwako Bwana.      Wewe ulinikomboa     kwa maumivu yako. 2.  Yesu nitakuimbia      hapa siku zangu zote.      Nitakapokumbuka,     neema na huruma zako.      Yesu nitakuimbia,      sababu wanilinda. 3.  Yesu nitakuimbia      katika maisha yangu.      Napenda kuingia      Bwana wangu unapokaa,      nikuimbie na malaika     milele na milele.

195. Mungu Awe Naye Daima

1.  Mungu awe naye daima,     hata tuonane tena,      awachunge kwa neema.     Mungu awe nanyi daima!            Na tukionana awepo,            na tuonane kwake!            Na tukionana awepo,            Mungu awe nanyi daima! 2.  Mungu awe nanyi daima.     Awafunike mabawa,      awalishe, awakuze.     Mungu awe nanyi daima!            Na tukionana awepo... 3.  Mungu awe nanyi daima,      awaonye kwa upendo      kaeni na kupatana.     Mungu awe nanyi daima!            Na tukionana awepo... 4.  Mungu awe nanyi daima,      awe kwenu na rehema      Zaeni matunda mema!     Mungu awe nanyi daima!           Na tukionana awep...

196. Upendo wa Mungu Wetu

1.  Upendo wa Mungu wetu      ndio jua letu.     Hutung’azia  moyoni      hufuta uchungu.     Giza hukoma na mchana     hutokea sasa,      furaha tupu na shangwe      huwamo moyoni.           Upendo huu una nguvu            tangu mwanzo na daima,           atupenda mimi nawe,            tuwe karibu na Yeye. 2.  Tangu mwanzo Baba Mungu      alivyotuumba,     ametuonyesha pendo     kwa kutukumbuka.      Hutupa mema mengi mno     duniani petu,     ila sisi hatukumpa      shukrani ya kweli.             Upendo huu … 3.  Ndipo akamtuma Yesu      mwenye pendo jingi.      Awaza, “Pendo la kufa,     watalikubali?”    ...

197. Ukimpata Mwenye Moyo

1.  Ukimpata mwenye moyo      mwaminifu daima,     umepata kito bora,      wajaliwa na Mungu.           Japo nimo shidani,          hali yangu ya heri.  2.  Ukiingiwa na taabu      na kupatwa na msiba,     mwenzi wako mwaminifu     atakutia moyo.            Japo nimo shidani  3.  Haja yake mwenzi huyu     kukusaidia tu.     Taabu yako ndiyo yake,      hakuachi msibani.              Japo nimo shidani... 4.  Rafiki wa duniani,      mali zitapotea,     mwenzi wako mwaminifu     atakaa kwa mpenziwe.              Japo nimo shidani …   5.  Mtu kuwa na mwenzake      mwaminifu daima,      ndiyo hali duniani     ...

198. Bariki Yote Yawe Mema

1.  Bariki yote yawe mema,     yote yawe mbaraka.      Watu wa nchi za dunia,      uwajaze utukufu.     Kaa kwetu, Bwana, bariki.      Uamini, wee ee ndugu      kweli yake Kristo.      Jaa utukufu wa Bwana     siku zako zote.          /:Vaa Mwokozi ee           na kweli yake, Haleluya./: 2.  Nyumba za wote zibariki     kwa Jina lako takata.      Ujaze utukufu wako,     nchi zote za dunia,             Kaa kwetu, Bwana … 3.  Nyosha mkono ubariki,     waliojiunga nawe.      Wakupokee maishani,     watunzwe nawe milele.              Kaa kwetu, Bwana … 4.  Bwana yatunze mambo yote     yaliyo mazuri kwako      Uwape wote wakuombao,     wafaniki...

199. Nikifa Nitapata Uzima kwa Yesu

1.  Nikifa nitapata      uzima kwa Yesu.      Ninampa moyo wangu,      nife kwa furaha. 2.  Napenda kwenda pale     alipo Bwanangu,     nikae mjini kwake      siku za milele. 3.  Nimeushinda sasa      uchungu na woga,     kwa damu ya Mwokozi     nimekombolewa. 4.  Zikipunguka nguvu,     pumzi ikiisha,      nisaidie Bwana,     nilale kwa raha. 5.  Saa yangu ikifika,     niiache dunia,      unitulize Bwana,      nichukue kwako.   6.  Nikifika mbinguni,      nitakuimbia      na kukusifu Bwana,      kwa furaha kubwa.

200. Sijui Saa ya Kufa Kwangu

1. Sijui saa ya kufa kwangu,    maisha yangu yapita.     Naomba Mungu, Bwana wangu    kwa ajili ya Mwanao.           Shika roho yangu,          kwa furaha,           niache ulimwengu huu.  2. Tukiwa hapa duniani     kufa kunatuvizia,     hakutuwekei kiaga,     kunakuja kwa haraka.             Shika roho … 3. Unifundishe nifikiri,    vizuri mambo ya kufa.     Nijutie makosa yangu,     yaondolewe na Yesu.              Shika roho …  4. Unipe nguvu, nijiweke    tayari kwa mambo yote.    Niweze kuitika vema,     ukiniita kwa kufa.              Shika roho … 5. Baba, ondoa dhambi zangu     kwa damu ya Bwana Yesu.    Naji...

201. Mwenzetu Kazi Yako Imekwisha

1.  Mwenzetu kazi yako      imekwisha duniani.      Umekwisha kutua      mzigo wa shida na taabu.           Yesu tupe kufika             walipo washindaji.   2.  Yesu ni kiongozi      katika bonde la kufa.      Amekutangulia      kaburini na peponi.            Yesu tupe …  3.  Wewe wachukuliwa     na malaika kwa Mwokozi.     Utapokewa sasa      na wateule wa Mungu.             Yesu tupe …  4.  Mwili wako wazikwa,      ugeuke kuwa vumbi.      Twatumaini kwamba      ufufuko utakuwa.             Yesu tupe …  5.  Sasa unapandwa tu     kama mbegu ya shambani.     Mpaka yaje mavuno      sik...

202. Watu wote Yawapasa

1.  Watu wote yawapasa      kufa kama majani.     Wakaao duniani,      yawapasa kuzikwa,      na kuoza kaburini,      wakitaka kugeuka      na kuona furaha,      tuliyoahidiwa. 2.  Hata mimi ni tayari,      nitamwekea Mungu      roho yangu akitaka,     kuniita kufani.      Kwani nimekombolewa     na Mwokozi wangu Yesu,     kufa kwake kuchungu      kumenipa tulizo. 3. Yesu amenikomboa    akinifia mimi.    Sasa mimi nitaacha     kwa furaha dunia,    na kuingia mbinguni     kwake Mungu Mwenye enzi,    na kwa Yesu Mwokozi     katika furaha kuu. 4. Kule wateule wengi     wanapomtumikia Mungu    penye kiti chake,    ni mahali pazuri.    Na malaika waimbapo   ...

203. Yesu Bwanangu Shujaa

1. Yesu Bwanangu shujaa     na Mwokozi anaishi.     Nikijua haya tu,    ninaweza kutuliza moyo wangu     ukiwa wenye woga wa kufa. 2. Yesu Mwokozi wangu,    Anaishi hata mimi     nitaishi mahali,     atakapokaa Bwanangu,     kwani viungo hukaa     palipo kichwa chao. 3. Nimeungana naye,     nikimtumaini yeye.    Ninamshika kwa nguvu,     nikimtegemea kweli.     Hata nguvu ya mauti     hainitengi naye. 4. Mwili wangu wa sasa    utaoza kuwa vumbi.    Baadaye na Yeye     atanifufua tena,    niwe mbinguni kwake     na kumwona milele. 5. Wenye unyonge hapa,     kule watapata nguvu.    Napandwa kwa aibu,     kule nina utukufu.    Ninapandwa kwa mwili,     nitaishi kwa roho. 6. F...

204. Wenye Mizigo Njooni

1. Wenye mizigo njooni,    nitawapumzisha.     Tusikilize sauti,    sauti yake Bwana.     Inatupa habari    ya baraka nyingi     dhambi huondolewa,     furaha inakaa. 2. Enyi wanyonge njooni,    nitawapa nguvu.    Wote sikilizeni     mbali na karibu!    Adui zetu wengi,     watupinga sana,    kwa nguvu ya Mwokozi     wote watashindwa. 3. Kila ajaye kwangu,     simfukuzi kamwe.     Sauti ya pendo hili    yatufurahisha.    Yesu aita wote     walio na dhambi,     wamjie wakapate     raha na mapenzi. 

205. Ametwaliwa Rafiki Yetu

1. Ametwaliwa rafiki yetu     hatutamwona tena mwilini.    Ameondolewa hapa petu,    tunamzika mwili kaburini. 2. Ametwaliwa tuliyempenda,    twajua ni mapenzi ya Mungu.    Hayupo kwani Mungu amwita,    aingie kundini pa Mungu. 3. Ametwaliwa kutoka kwetu,     lakini tutaonana tena.    Yu katika furaha ya kweli,     na kule tutaimba pamoja!

206. Kuna Nchi Nzuri Mbali Sana

1. Kuna nchi nzuri mbali sana.    Wako watu wema, wasimama,    waimba vizuri sifa zake     Mwokozi,    nasi duniani twamtukuza. 2. Njooni kwa nchi hii njooni sasa!    Mbona mwasimama    mashakani?    Tuache makosa,    yanamchukiza Bwana.     Kwake tutaketi kwa salama. 3. Machozi hapana,     wala hamu,    mbele yake Baba     mapenzi tu.    Utaona raha utapewa     kilemba kuvikwa na wale wa     mbinguni!

207. Lala Rafiki, Lala Mpenzi

1. Lala rafiki, lala mpenzi     laza kichwa chako kwa Mwokozi.    Lala vyema, lala usingizi,          lala, lala vyema. 2. Aa! mpenzi sisi twakupenda,    si kama akupendavyo Bwana.    Mapenzi yake yazidi sana.          Lala, lala vyema. 3. Ulivyolala ni kama mwana     huamki kwa taabu tena.     Raha kule utulivu sana.        Lala, lala vyema. 4. Hata jua tukufu litoke    hata watu wema wafufuke.    Waje na Yesu waume, wake.            Lala, lala vyema. 5. Siko kuagana, si ‘kwa heri’    punde atakuja tumkiri.     Uwe mmoja kwake wa heri.           Lala, lala vyema. 6. Mpaka tuonane mbele zake,     na mavazi awapayo wake.    Hata ya siri yafunuliwe.           Lala, lala vyema

208. Ee Moyo Wangu Amka

1. Ee moyo wangu amka,     mwimbie Mwumba wako,    aliyetupa neema,     atulindaye sote. 2. Nilipolala leo,    usiku wewe Baba     umenilinda vema,    sikuwa na hatari. 3. Wasema: “Mtoto wangu,     usiogope kitu,    ulale usingizi,     nitakuamsha kesho” 4. Nimevipata vile    ulivyoniambia.    Naona mchana tena     na nguvu na uzima. 5. Nilipe jinsi gani     ulivyonitendea?    Nakupa moyo wangu    sina kizuri zaidi. 6. Huwezi kukataa     kipaji kama hicho.    Wajua kama sina    mengine ya kukupa. 7. Maliza kazi yako     uliyoanza kwangu,    tuma malaika wako     anikingie msiba. 8. Kubali nitendayo,     unipe shauri jema,    kuanza na kuisha    ni shauri lako, Bwana. 9. Unibariki leo,   ...

209. Jua Likicha Linanyang’aza

1. Jua likicha linayang’aza    mashamba yetu kwa     utukufu wa nuru yake    yenye neema kuu.    Nimelegea maungo usiku;     sasa ni macho, naona furaha    nikitazama viumbe vyote. 2. Njooni tuimbe tukamtolee    Muumba sadaka za mioyo yetu,    mambo mazuri tuliyo nayo.    Mungu ataka mioyo ya watu,    nyimbo za sifa na za     kumshukuru,    ndizo sadaka zimpendezazo. 3. Kazi ya Mungu ni kila siku     kutubariki, kutuongoza,    kutukingia hatari nyingi,    sisi twalala, Bwana anakesha;    tukiondoka, anatung’azia    mwanga mzuri wa huruma yake. 4. Mambo ya watu, yote yapita.    Mambo ya Mungu yanasimama.    Neno la Bwana lakaa milele.    Atutolea wokovu wa neema,    ayaondoa machungu ya kufa,    tuwe wazima hapa na huko. 5. Mwenye huruma unisamehe ...

210. Kila siku Asubuhi

1. Kila siku asubuhi    Yesu anabisha hodi     mlangoni kwa wamwombao:    Bwana Yesu, njoo kwetu! 2. Tumfungulie milango     ya mioyo aingie,     Tumwalike kwa furaha:    “Bwana Yesu, njoo kwetu”. 3. Kaa kwetu siku zote,     ufukuze maadui,     wasiweze kutudhuru     sisi tulio wako. 4. Uwe Mchunga wetu mwema,    utulishe malishoni,     tukutumaini wewe     leo na siku zote. 5. Kweli Yesu atulisha,    anatuongoza leo.    Ni furaha yetu kubwa.    Tunakwenda na Yesu. 

211. Muumbaji wa Vitu Vyote

1.  Muumbaji wa vitu vyote      Baba, Mwana na Roho,      uletaye kila siku,     jua, mwezi, na nyota,      ulindaye vizuri       viumbe vyako vyote. 2.  Ninakushukuru Baba,     kwamba umenilinda,      ukanikingia tena      shida, woga, huzuni,     hata hila ya mwovu      haikunipoteza.  3.  Niongoze Bwana wangu,      kwa nenolo siku hii.     Uwe mlinzi wangu leo,     nisikose kukutii.     Usiponiongoza      sina budi kukosa. 4.  Umtume malaika wako      anishike vizuri,      akazizuie hila,     majaribu na tamaa.     Naye anichukue     mwisho kwako mbinguni.

212. Bwana Twakuomba Sasa

1. Bwana twakuomba sasa,    tutokee sisi hapa,    kwani siku yako leo.    Tupe, kufikiri vema     Neno lako la uzima,     na la ukombozi wetu     sisi tuliopotea     tupate kurudi kwako. 2. Yawe mbali kwetu sasa     kila mambo masumbufu.     Roho na mioyo yetu     ikaongee na Mungu.     Tupate kutiwa hamu     ya raha iliyo kwako,    itakayotutokea     baada ya maisha haya. 3. Naona kitini pako     taji lao washindao;     nasikia nyimbo zao     waishao kupigana.     Hao wakusifu wewe    kwa zaburi na kwa shangwe.    Hata mimi nijalie     nipate kufika kule. 4. Upungufu wangu wote     ufunike wewe Bwana;     niwe mtakatifu wako    duniani hapa chini,     ...

213. Nakushukuru Mungu

1. Nakushukuru Mungu    kwa kinywa na moyo     saa hii ya asubuhi     hata siku nzima.     Nitakuimbia, nitakusifu Baba,    alivyonifundisha     Mwanao wa pekee.  2. Umenilinda Bwana,    usiku kucha huu     ukaondoa shida,     hatari na msiba.     Nakuomba sasa:      Uondoe makosa     niliyokukosea     kwa neno na tendo. 3. Nilinde hata leo     kwa neema yako tu,    asinishinde mwovu     kwa hila yake kuu.    Nisione shida     ya moto na ya maji,     ya homa na ugonjwa,    ya kufa kubaya.   4. Mungu atanitunza     aliye Mwenyezi,     ayabariki yote nitakayotenda.    Namwekea Yeye     uzima hata kufa,    anitendee yale    yanayompende...

214. Tokea Nuru ya Mchana

1. Tokea nuru ya mchana,     uamshe mwili na roho    kwa mwanga wako mzuri.    Tokea nuru ya roho,    niimbe wimbo wa sifa     wa kumshukuru Mungu.     Mwimbieni kwa furaha    Mwenye enzi alindaye    na kuwabariki watu. 2. Ninakushukuru Mungu    kwa moyo wote sababu     ya neema yako kubwa.    Umenilinda usiku    mwili na roho vizuri     kwa jeshi la malaika.     Nikaweza kuondoka     kitandani kwa furaha     mwenye nguvu na uzima.   3. Ninakuomba Babangu,    uyaondoe makosa,    hofu na shida kwangu.     Niamke hata rohoni,    kwa neema yako na pendo    nitakutumikia.    Niongoze nifikiri,    mambo yangu mbele yako,    nipate baraka yako. 4. Ee Yesu, uniongoze    nishike njia yako tu  ...

215. Tumsifu Bwana Sote

1. Tumsifu Bwana sote tumpendao     tumshangilie kwa furaha kubwa     na kumtolea sifa na shukrani.     Tumsifu Bwana! 2. Aliyelinda nguvu na uzima     aliyetupa Yeye leo tena.     Ametuamsha wenye hali njema.    Tumsifu Bwana! 3. Tukitumia nguvu za maungo,    tukisikia na kusema sawa    ndio baraka na huruma yake.    Tumsifu Bwana! 4. Mchungaji mwema,     atupaye yote,    twaomba: Utulinde hata leo,    tuone wingi wa rehema yako.     Tumsifu Bwana!   5. Tusaidie, tufuate leo    kwa nguvu zako     njia za kunyooka,     tusikuache na rehema yako.    Tumsifu Bwana! 6. Utufundishe kusikia Neno     na kulishika     kwa mwenendo mzuri.     Tusaidie tulio wanyonge.    Tumsifu Bwana! 7. Utuongoze,  tusikose njia  ...

216. Babangu Kule Mbinguni

1. Babangu kule mbinguni,     aliye juu pa malaika,           /: aangalia njia zangu             na kunilinda maisha. :/ 2. Hata unywele kichwani    hauanguki ovyo tu          /: na siri zote za moyoni            zajulikana kwa Baba. :/ 3. Zamani nisipojua,     amekwisha kuandika          /: mkononi mwake jina langu,             ndio upendo wake mkuu.:/ 4. Ee Baba yangu u mwema,    nami nataka kufanya          /: kama malaika wafanyavyo             mbinguni kwako milele!:/ 

217. Ee Yesu Mesiya

1. Ee Yesu Mesiya,    Usiku umekwisha.    Mwanga wa huruma,     wanizunguka tena.     Vyote vimeamka,     vyakusifu wewe,    hata mimi Yesu,    ninakutukuza! 2. Ninaamka sasa     nazivaa nguo zangu,    hata roho yangu,     uipambe mwenyewe,     wongofu na pendo     na uvumilivu viwe pambo langu,    univike hivyo! 3. Uliye popote ukae hata kwangu,     nilinde kwa wema     katika njia zangu!     Nikusifu wewe    kwa mwenendo wangu,     kwa neno na tendo     siku zangu zote. 4. Nakuomba tena: Uzibariki vema    kazi zangu zote     ninazofanya leo!     Naye Roho wako    atawale kwangu,     niwe mtoto wako     hapa na huko juu.

218. Pambazuko la Jua

1. Pambazuko la jua,    mwanga usiopimika,     unapotutokea     tunaamshwa na moyoni.    Giza linafukuzwa na mchana. 2. Umande unanyesha     yatakayo kunyauka,    nami nione kwako     nguvu kuinuka tena,     niongozwe rohoni kwa kweli. 3. Asubuhi uzima     unaletwa duniani,     nami ninatamani     kufufuka na rohoni,     ufufuke na mwili mbinguni. 4. Mchana zinaangazwa     njia zote kwa furaha,     woga unapokwisha    na machozi na mashaka,     ndipo nitachangamka daima.

219. Asubuhi na Mapema

1. Asubuhi na mapema nakukaribia,     kukushukuru, ee Bwana,     kwa uzima wangu. 2. Uliyenipa usiku kulala ni mzima,    nakuomba sasa, Mungu,     unilinde mchana. 3. Nilinde majaribuni,    kwani sina nguvu,     hivi leo maovuni     uwe ngao yangu!   4  Katika maneno yangu     nisiseme uongo,    macho yako Bwana Mungu,    yanitunze mimi! 5. Njia yangu nipitayo     wewe uwe nami,    kila niendako leo     uwe kiongozi!

220. Naamka Mimi Tena

1.  Naamka mimi tena      kwa nguvu na afya.     Na moyo wangu Baba,      wakusifu wewe. 2.  Baraka na furaha      popote zimejaa,     zatoka kwako wewe      zimetuingia. 3.  Twaimba sifa zako     kwa mioyo na vinywa,     miti, wanyama wote,      wakusifu Bwana. 4.  Na sisi twapaliza      sauti zetu sasa,     maisha yetu yote     yawe sifa pia! 

221. Ee Bwana Mungu Mkuu

1. Ee Bwana Mungu Mkuu    uliye muumbaji,    Yesu uliye mwenye fahari,    ninajitolea sasa na milele     nakupa roho na mwili wangu    maisha yangu nakupa wewe,    vyote na vyote vilivyo vyangu,    ninakutolea kwa furaha. 2. Mionzi ya jua    na mwanga wa mwezi    vyatoka nuruni mwako Yesu.    Na jeshi la nyota     ndilo taji zuri     kichwani kwako     Mfalme wa mbingu.    Vyote na vyote ulimwenguni    asili yao kwako ee Yesu;     vyote vyahubiri ukuu wako. 3. Umechaguliwa kuwa kimbilio     la watu wenye shida na     dhambi.    We wasaidia, dhambi waondoa,    japo mashaka yakiwa mengi,    hatari zote watukingia.    Jeshi la adui utalishinda     kwa nguvu yako kuu     ya kimbingu. 4. Toka duniani twakuelekez...

222. Bwana, Imepita Tena

1. Bwana, imepita tena    siku moja ya neema.     Nifundishe nifikiri    mambo yote ya leo.    Unionyeshe sasa     niliyokukosea.     Nimalize mambo yote    kad’ri ya mapenzi yako.  2. Kweli utaona mengi     yasiyokupendeza.     Kwani ni mtu wa makosa,    yaliyo mengi sana.    Moyo wangu, na kinywa,    na mikono yakosa    kwa kuwaza na kusema     na kutenda kila siku.   3. Nakuomba ewe Mungu    nihurumie tena.    Ondoa maovu yote    niliyokutendea.     Uyafute makosa    kwa rehema yako kuu.     Nitaangalia kesho     nizishike amri zako.  4. Bwana wewe unakesha,     sisi tukisinzia.    Macho yako hayachoki,    ndiwe Mchungaji mwema,    awalindaye kondoo     katika...

223. Jioni Moyo Wangu Wakutafuta

1. Jioni moyo wangu     wakutafuta Bwana,     na kukushukuru.     Unikazie macho     yenye baraka nyingi,     ung’aze mwili na roho. 2. Natumaini tena     rehema yako Baba     hata usiku huu.     Fukuza majaribu     na hila ya Shetani,    ukiwa karibu yangu. 3. Unanipenda sana,    wakaa pamoja nami,     wanikaribisha.     Unanifurahisha    kwa wema wako mwingi,     sababu hii nakusifu. 4. Maisha yanapita     upesi, ni safari     ya kwenda mbinguni.    Unifundishe, Bwana,     kuelekea kwako:     Pazuri ni mbinguni tu. 

224. Kukichwa Watu Wote

1. Kukichwa watu wote    na wanyama nyumbani     na ndege walala.    Ee moyo wangu sasa     uanze kufikiri     ninavyompendeza Mungu. 2. Jua limeingia, Giza limetokea,     usiku karibu.     Jua lingine sasa     lang’aza moyo wangu:    Ni Yesu, Mwokozi wangu. 3. Miguu hata mikono     inafurahi sana, kazi imekwisha.    Nao moyo wataka     kukombolewa hivyo    katika nguvu za mwovu. 4. Nafumba macho yangu,     nalala usingizi, sijui lolote.    Wewe uangalie    roho na mwili wangu,    uliye mlinzi wetu mkuu. 5. Yesu furaha yangu,     unifunike sasa, unikumbatie.    Uagize malaika     wanikingie shida,    Shetani akinitaka. 6. Hata wapenzi wangu     nawaombea wote     wasione shida.     ...

225. Mchunga Wangu Mwema

1. Mchunga wangu mwema,     huna usingizi unakesha tu.    Baba, nimeona     neema yako leo     mchana kutwa huu.    Hata na usiku huu     utawatuma malaika,     wanilinde mimi. 2. Uwalinde tena    baba na mamangu,     nao ni wako.     Utufiche sisi    mikononi mwako,    tusiogope!    Njoo Bwana, tuungane:    mimi kwako, nawe kwangu    hivyo nitalala.   3. Linda mlango wangu    na huzuni zangu niondolee.    Unikumbatie ndani ya    mabawa yako nilale.     Unifiche vizuri:    ndivyo mwovu hataweza     kunikaribia. 4. Baba, ukitaka     kuniita mimi leo usiku,    nitaweka roho     mikononi mwako uipokee.    Nitalala kwa raha,     kwani wewe wanilinda     leo...

226. Nimechoka Kabisa

1.  Nimechoka kabisa     macho yangu mazito;      macho yako Babangu,      yanilinde usiku. 2.  Niliyokukosea,      Mungu niondolee!       Damu ya Yesu Kristo     huning’aza kabisa 3.  Ndugu zangu, ee Mungu,     uwalinde usiku;      wakubwa na wadogo     wote walale raha. 4.  Wenye shida tuliza,     uwafute machozi,      uwapokee wote      wafao usiku huu. 

227. Kaa Nami ni Usiku Tena

1.  Kaa nami, ni usiku tena;     Usiniache gizani, Bwana;      Msaada wako haukomi;      Nili peke yangu, kaa nami. 2.  Siku zetu hazikawi kwisha,     Sioni la kunifurahisha;      Hakuna ambacho hakikomi,     Usiye na mwisho, kaa nami. 3.  Nina haja nawe kila saa;      Sina mwingine wa kunifaa;      Mimi nitaongozwa na nani     Ila Wewe? Bwana, kaa nami. 4.  Sichi neno uwapo karibu;      Nipatalo lote, si taabu;     Kifo na kaburi haviumi;      Nitashinda kwako, kaa nami. 5.  Nilalapo nikuone wewe,     Gizani mwote nimulikiwe;     Nuru za mbinguni hazikomi,      Siku zangu zote kaa nami.

228. Jua Limekuchwa

1. Jua limekuchwa, waja usiku,    twakaa na Yesu rohoni mwetu. 2. Nyota zatokea, ndege watua,    kazi imekwisha, mwili walala. 3. Bwana ukumbuke wakuitao,    ukawatulize na waumwao. 4. Ndoto za watoto zitoke kwako,    tukifumba macho, utubariki! 5. Wasafiri bara na baharini,    linda, wazuie na wakosaji! 6. Hata asubuhi tunapoamka,    upendezwe nasi, tukikushika.