164. Tumekujia Bwana Wetu

1. Tumekujia Bwana wetu 

   kujiweka mkononi mwako,

   tuwe wako hata milele

   twakushukuru na twakusifu.

   Mwokozi wetu, utukubali, 

   utuongoze njia ya mbingu.


2. Twataka kubatizwa leo 

   kwa Jina lako, tuwe Wakristo.

   Umetukomboa na sisi 

   ulipokufa pale Golgota, 

   na kwamba wewe upo karibu,

   unasikia kuomba kwetu.


3. Twakupambia mioyo leo, 

   ingia, Mfalme wa utukufu!

   Utupe sisi nuru yako

   tuwe mwanga katika dunia.

   Pokea leo mioyo yetu, 

   tunajitoa kwako wenyewe.


4. Tunakuomba sasa, Bwana,

   usitutie majaribuni. 

   Utuongoze siku zote, 

   tukufuate wenye imani.

   Mwisho tufike kwenye enzi kuu,

   tuipokee taji ya mbingu.

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima