182. Nuru ya Rohoni

1. Nuru ya rohoni ni Bwana Yesu.

   Nakuomba sana niangazishe; 

   ukanitazame kwa huruma tu, 

       /: Ukanitulize    

        mimi maskini. :/


2. Futa dhambi zangu 

   kwa damu yako. 

   Hasira ya Mungu iniondoke. 

   Machubuko yako, hata mateso,

       /: Niyawaze vema  

        rohoni mwangu. :/ 


3. Nakutumaini peke yako tu,

   niwe mtumwa wako 

   pote nilipo, utanikubali, 

   sina mashaka!  

      /: Nitakushukuru 

        pasipo mwisho. :/

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima