174. Ewe Baba, Bwana wangu
1. Ewe Baba, Bwana wangu,
nielekeze mwenendo
nifuate Neno lako
hata leo kaa kwangu!
Uwe mlinzi na ngao
uongoze maisha mpaka nifike
kwako!
2. Umenipa na wazazi
walio mkono wako,
wanifundisha vizuri,
hata na wadhamini,
walimu na wakuu
Baba Mungu naomba
nao uwaongoze!
3. Hata ndugu zangu wote
umenipa kwa wema,
nisaidiane nao
siku zote kwa pendo.
Utupe kuungana
wakubwa tuheshimu
kwa maneno mazuri!
4. Ulikuze kundi letu
tukae na adabu,
tuinue nchi yetu
siku zitungojazo!
Nao ufalme wako
uenezwe na kwetu,
uheshimiwe! Amen.
Comments
Post a Comment