213. Nakushukuru Mungu
1. Nakushukuru Mungu
kwa kinywa na moyo
saa hii ya asubuhi
hata siku nzima.
Nitakuimbia, nitakusifu Baba,
alivyonifundisha
Mwanao wa pekee.
2. Umenilinda Bwana,
usiku kucha huu
ukaondoa shida,
hatari na msiba.
Nakuomba sasa:
Uondoe makosa
niliyokukosea
kwa neno na tendo.
3. Nilinde hata leo
kwa neema yako tu,
asinishinde mwovu
kwa hila yake kuu.
Nisione shida
ya moto na ya maji,
ya homa na ugonjwa,
ya kufa kubaya.
4. Mungu atanitunza
aliye Mwenyezi,
ayabariki yote nitakayotenda.
Namwekea Yeye
uzima hata kufa,
anitendee yale
yanayompendeza.
Comments
Post a Comment