186. Mfalme wa Upendo Ndiye

1. Mfalme wa upendo ndiye 

   anichungaye mimi,

   Yeye ni wangu milele,

   ananipenda daima.


2. Kwenye maji ya uzima 

   hunipeleka mimi

   katika malisho mema, 

   anilisha siku zote.


3. Mara nyingi napotea

   kwa ukaidi wangu, 

   naye ananitafuta, 

   na kunirudisha kwake.


4. Kivuli cha kufa kwangu 

   sitaogopa tena,

   ukiwa kwangu daima 

   mashaka wayaondoa.


5. Wanitandikia meza, 

   naula mkate wako, 

   nanywa katika kikombe

   nikumbuke kufa kwako. 


6. Siku zangu zote hapa  

   wema wako u vivyo.

   Nikubali Mchunga mwema,

   nikuimbie milele.


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima