217. Ee Yesu Mesiya

1. Ee Yesu Mesiya,

   Usiku umekwisha.

   Mwanga wa huruma, 

   wanizunguka tena. 

   Vyote vimeamka, 

   vyakusifu wewe,

   hata mimi Yesu,

   ninakutukuza!


2. Ninaamka sasa 

   nazivaa nguo zangu,

   hata roho yangu, 

   uipambe mwenyewe, 

   wongofu na pendo 

   na uvumilivu viwe pambo langu,

   univike hivyo!


3. Uliye popote ukae hata kwangu, 

   nilinde kwa wema 

   katika njia zangu! 

   Nikusifu wewe

   kwa mwenendo wangu, 

   kwa neno na tendo 

   siku zangu zote.


4. Nakuomba tena: Uzibariki vema

   kazi zangu zote 

   ninazofanya leo! 

   Naye Roho wako

   atawale kwangu, 

   niwe mtoto wako 

   hapa na huko juu.


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima