207. Lala Rafiki, Lala Mpenzi
1. Lala rafiki, lala mpenzi
laza kichwa chako kwa Mwokozi.
Lala vyema, lala usingizi,
lala, lala vyema.
2. Aa! mpenzi sisi twakupenda,
si kama akupendavyo Bwana.
Mapenzi yake yazidi sana.
Lala, lala vyema.
3. Ulivyolala ni kama mwana
huamki kwa taabu tena.
Raha kule utulivu sana.
Lala, lala vyema.
4. Hata jua tukufu litoke
hata watu wema wafufuke.
Waje na Yesu waume, wake.
Lala, lala vyema.
5. Siko kuagana, si ‘kwa heri’
punde atakuja tumkiri.
Uwe mmoja kwake wa heri.
Lala, lala vyema.
6. Mpaka tuonane mbele zake,
na mavazi awapayo wake.
Hata ya siri yafunuliwe.
Lala, lala vyema
Comments
Post a Comment