183. Usiku Ulipotolewa
1. Usiku ulipotolewa,
Yesu, umetugawia
mapato ya mateso yako,
tukumbuke kufa kwako.
Waaminio wakusifu
wakija karamuni kwako.
2. Tunakumbuka kufa kwako,
tukila mwili wako huu;
twapewa nguvu ya uzima
tukinywa damu yako hii.
Karamu hii tunayopewa
yatuonyesha pendo lako.
3. Huu mkate ni chakula kweli,
hii damu yatutuliza;
mioyo yetu yapumzishwa
tukila mezani kwako.
Tunaongezwa nguvu zetu,
za kukutegemea vema.
4. Twashirikiana na wote
walio viungo vyako;
kwani tunashibishwa sote
kwa mwili na damu moja,
tu kundi la Mchungaji mmoja;
kwa hivi twapatana sote.
5. Twapewa mwili wako Bwana,
tujue kweli ya kwamba
miili yetu ya unyonge
itageuka vizuri.
Tutapokea mwisho kwako
miili mipya ya uzima.
6. Watupa mema mengi
Bwana Mwana Kondoo wake
Mungu,
mwenyewe u chakula chetu,
kweli twatunzwa vizuri.
Twakila hapa kwa uchungu,
lakini kwako kwa furaha.
Comments
Post a Comment