209. Jua Likicha Linanyang’aza
1. Jua likicha linayang’aza
mashamba yetu kwa
utukufu wa nuru yake
yenye neema kuu.
Nimelegea maungo usiku;
sasa ni macho, naona furaha
nikitazama viumbe vyote.
2. Njooni tuimbe tukamtolee
Muumba sadaka za mioyo yetu,
mambo mazuri tuliyo nayo.
Mungu ataka mioyo ya watu,
nyimbo za sifa na za
kumshukuru,
ndizo sadaka zimpendezazo.
3. Kazi ya Mungu ni kila siku
kutubariki, kutuongoza,
kutukingia hatari nyingi,
sisi twalala, Bwana anakesha;
tukiondoka, anatung’azia
mwanga mzuri wa huruma yake.
4. Mambo ya watu, yote yapita.
Mambo ya Mungu yanasimama.
Neno la Bwana lakaa milele.
Atutolea wokovu wa neema,
ayaondoa machungu ya kufa,
tuwe wazima hapa na huko.
5. Mwenye huruma unisamehe
makosa yangu, uyaondoe
machoni pako kwa neema yako.
Tena naomba: Nilinde vizuri,
uniongoze na kunitawala
kama mwenyewe
unavyopenda.
6. Msiba na shida mwisho zapita;
kama twaona mwanga wa jua
baada ya mvua mbinguni tena.
Raha, uzima, furaha, amani
zaningojea mbinguni kwa
Mungu:
Ninatamani furaha za juu.
Comments
Post a Comment