155. Ondokeni! Tunaitwa

1. Ondokeni! tunaitwa 

   na walinzi wa juu 

   mnarani 

   Yerusalemu, amka wee! 

   Ni usiku wa manane,

   yuaja Bwana wa arusi, 

   wanawali wako wapi? 

   Amkeni upesi! 

   Kaziwasheni taa. 

   Haleluya!

   Fuateni arusini 

   kwenda kumpokea 

   Bwana!


2. Sayuni anasikia, 

   moyo waruka kwa furaha, 

   yu macho anaondoka.

   Mponya wake anashuka 

   mbinguni mwenye 

   utukufu, 

   aleta mwanga wa kweli, 

   taji yake yaja

   na Mwana wa Mungu. 

   Hosiana!

   Twafuata kwenye shangwe 

   tukale karamu yake.


3. Waimbiwa nyimbo nzuri 

   kwa misemo ya watu wote 

   na ya malaika mbinguni.

   Tukifika mjini kwako

   kwenye milango ya malulu

   tutakuimbia nasi.

   Furaha kama hii 

   haijasikiwa duniani.

   Nasi sasa tunaimba,

   tunakusifu, Ee Bwana. 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima