154. Ninataka Kuingia

1. Ninataka kuingia 

   mjini kwa Mungu. 

   Nitashinda, nitakaza 

   mwendo nifike, 

   nikishikwa na shida,

   nikichoka njiani, 

   Yesu unaniambia: 

   “Uningojee!”


2. Naitwa na Yesu Kristo

   enzini mwake.

   Nakimbia, kukawia 

   hakuna faida,

   wote wachelewao 

   hawatapata taji. 

   Mimi sitaki kingine 

   ila uzima.


3. Elekeza macho yangu

   mlangoni pako. 

   Niongoze, nipe nguvu, 

   ninapochoka. 

   Ninapojaribiwa, 

   ninaposingiziwa,

   Yesu, unisaidie 

   nisikuache.


4. Mkono wako 

   unishike nisianguke.

   Najiona kuwa mnyonge,

   nguvu i kwako,

   Neno lako, ee Yesu, 

   linanipa uzima. 

   Nikifika, nitaimba,

   “Umeniponya!”

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima