179. Yesu Kwa Imani
1. Yesu kwa imani, nakutumaini,
peke yako.
Nisikie sasa na kunitakasa,
ni wako kabisa tangu leo.
2. Nipe nguvu pia za kusaidia
moyo wangu.
Ulikufa Wewe, wokovu nipewe,
nakupenda Wewe,
Bwana wangu.
3. Hapa nazunguka
katika mashaka, na matata.
Palipo na giza utaniongoza
hivi nitaweza kufuata.
4. Takuwa mzima
nivushe salama mautini.
Sina hofu kamwe
ukiwapo nami,
nami nikwandame siku zote.
Comments
Post a Comment