176. Tumiminie ee Mtakatifu

1. Tumiminie ee Mtakatifu, 

   Roho wako mwenye nguvu

   atakase mioyo yetu, 

   tuwe wako tu kale na kale!


2. Wewe mwenyewe, 

   tulinganishe

   tuungame kwa furaha,

   ya kuwa u Bwana wetu,

   tena Mwokozi

   kwa damu yako!


3. Tukutazame 

   kwa mioyo yote,

   tukilirudisha upya 

   agano la ubatizo,

   tukufuate, tuache yetu!


4. Tukija sasa kubarikiwa,

   sikia kuomba kwetu, 

   tugawie mema mengi, 

   tutengemane 

   mwangani mwako!


5. Na atujie Roho wa Bwana,

   atuunganishe sote 

   kuwa kundi takatifu 

   mpaka tumwone 

   kwake mbinguni! 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima