202. Watu wote Yawapasa
1. Watu wote yawapasa
kufa kama majani.
Wakaao duniani,
yawapasa kuzikwa,
na kuoza kaburini,
wakitaka kugeuka
na kuona furaha,
tuliyoahidiwa.
2. Hata mimi ni tayari,
nitamwekea Mungu
roho yangu akitaka,
kuniita kufani.
Kwani nimekombolewa
na Mwokozi wangu Yesu,
kufa kwake kuchungu
kumenipa tulizo.
3. Yesu amenikomboa
akinifia mimi.
Sasa mimi nitaacha
kwa furaha dunia,
na kuingia mbinguni
kwake Mungu Mwenye enzi,
na kwa Yesu Mwokozi
katika furaha kuu.
4. Kule wateule wengi
wanapomtumikia Mungu
penye kiti chake,
ni mahali pazuri.
Na malaika waimbapo
nyimbo za kumsifu Bwana:
Ee Mungu Mtakatifu,
Baba, Mwana na Roho.
5. Waliko wazee wa kale,
wafumbuaji wa Mungu;
kule wanakaa mitume
juu ya viti vya enzi;
kule wamekusanyika
waliotutangulia,
kule tutasikia
Haleluya daima.
6. Naona Yerusalemu
unang’aa kwa mwanga mkuu
Nasikia sauti nzuri
za vinubi na nyimbo.
Kweli ni furaha kubwa,
kule jua litokapo
unapopambazuka
mchana usioisha.
7. Nimeona haya yote
rohoni kwa furaha.
Basi ninapenda kwenda
kuingia mbinguni!
Ndugu zangu: Kwaherini!
Mungu awalinde nyote.
Kwaherini! Nakwenda,
imekwisha safari
Comments
Post a Comment