184. Moyo Wangu Ujipambe
1. Moyo wangu ujipambe,
acha mambo ya gizani.
Kaza mwendo wa nuruni
hivi utang’aa vizuri.
Kwani Bwana wa rehema
akukaribisha kwake.
Mwenye utukufu mwingi
anapenda kuja kwako.
2. Amka ukamlaki yeye,
umkaribishe vizuri.
Abishaye hodi kwako,
akuleteaye neema.
Umkubali kwa furaha
aingiaye moyoni.
Sema: Bwana, nakupenda,
sikuachi siku zote.
3. Hatuwezi kufahamu
mambo haya ya ajabu:
Unapenda kuwa nasi
kwa mkate na kwa mvinyo.
Yesu, tunaomba sana:
Wewe kaa leo hapa,
tugawie neema yako,
Chakula Kitakatifu.
4. Yesu, jua la rehema,
Yesu,chemchem ya uzima,
Yesu, nakupenda sana,
nuru ya maisha yangu.
Nakuomba: nibariki
nikila chakula chako
nipe nguvu ya uzima,
tuishi wewe na mimi.
5. Pendo limekuhimiza
kutafuta wakosaji.
Umetoa mwili wako
kutulisha roho zetu,
ukamwaga damu pia
ili utunyweshe sisi.
Twakumbuka pendo hili
hapa karamuni kwako.
6. Yesu, mkate wa uzima,
nijalie nisikose
msaada wa karamu yako,
nisijiponze nikila.
Nikumbuke, mambo haya
yaonyesha pendo lako.
Unisaidie, niwe
mgeni wako kwa milele.
Comments
Post a Comment