194. Yesu Nitakuimbia

1.  Yesu nitakuimbia

    kwa rehema zako zote.

    Baraka nyingi sana 

    nimepata kwako Bwana. 

    Wewe ulinikomboa

    kwa maumivu yako.


2.  Yesu nitakuimbia 

    hapa siku zangu zote. 

    Nitakapokumbuka,

    neema na huruma zako. 

    Yesu nitakuimbia, 

    sababu wanilinda.


3.  Yesu nitakuimbia 

    katika maisha yangu. 

    Napenda kuingia 

    Bwana wangu unapokaa, 

    nikuimbie na malaika

    milele na milele.


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima