204. Wenye Mizigo Njooni

1. Wenye mizigo njooni,

   nitawapumzisha. 

   Tusikilize sauti,

   sauti yake Bwana. 

   Inatupa habari

   ya baraka nyingi 

   dhambi huondolewa, 

   furaha inakaa.


2. Enyi wanyonge njooni,

   nitawapa nguvu.

   Wote sikilizeni 

   mbali na karibu!

   Adui zetu wengi, 

   watupinga sana,

   kwa nguvu ya Mwokozi 

   wote watashindwa.


3. Kila ajaye kwangu, 

   simfukuzi kamwe. 

   Sauti ya pendo hili

   yatufurahisha.

   Yesu aita wote 

   walio na dhambi, 

   wamjie wakapate 

   raha na mapenzi. 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima