158. Liko Pumziko la Mioyo

1.  Liko pumziko la mioyo, 

    amka wee unayechoka, 

    Unaugua kama mfungwa kwa

    shida za moyo wako 

    Umtazame Kondoo wa Mungu 

    atakuchunga kwa furaha.

    Uache mzigo enenda. 

    Vita nzuri yamalizika,

    safari yabaki kidogo 

    inayokusumbua mno.


2.  Mungu ametuchagulia 

    pumziko lisilo mwisho

    Amelitengeneza kale, 

    mtu hajazaliwa bado, 

    kufa kwamfurahisha  Mponya,

    tupate pa kupumzikia. 

    Aita, anaalika 

    mioyo inayokaa na shida, 

    msikawie, njooni leo!

    Ingieni pumzikoni!


3.  Ninyi mshindwao na mizigo

    mlemewao na uzito 

    Rukeni kimbieni hima, 

    tokeni pangoni mwenu;

    msienende kwa kuinama,

    Mponya anawaambieni: 

    Mimi ni pumziko lenu, 

    ninyi wana wote wa Mungu.

    Popote mwalizwa na shida,

    kwa Yesu mwanyamaa kimya!


4.  Hapo pumzikeni rahani,

    wasiwasi hatunao. 

    Shikeni Neno hili jema: 

    Pumzikeni, Yesu yuko! 

    Shikeni mabawa upesi, 

    karukieni kama ndege 

    Wako jamaa wanangoja; 

    Furahi moyo, shangilia,

    patana nao utukuze,

    uko mwaka wa pumziko!


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima