163. Mungu Upokee Moyo Wangu
1. Mungu upokee
moyo wangu wote,
niwe mtoto wako,
siku zangu zote.
Nikufuate Wewe
nisikuache tena,
nishike siku zote,
ulivyotuagiza.
Unisaidie mimi,
hata kufa kwangu.
2. Msalabani pako,
Yesu naanguka,
uliyenifia
hata mimi pia.
Yaondoe makosa
yatoweke kabisa,
nipate kuwa safi
kwa damu yako bora.
Unisaidie mimi
hata kufa kwangu.
3. Roho Mtakatifu,
unanipa nguvu;
niweze kushinda
majaribu yote,
naomba: utawale
katika moyo wangu,
Shetani, hata kufa,
asinishinde mimi.
Unisaidie mimi,
hata kufa kwangu.
4. Baba, Mwana, Roho
uliye mmoja tu,
niliye maskini
nakuomba sana:
Unikubali sasa,
katika ubatizo,
futa makosa yangu
kwa maji haya bora.
Unisaidie mimi,
hata kufa kwangu.
Comments
Post a Comment