185. Bwana Wetu Ametoa

1. Bwana wetu ametoa 

   mara moja msalabani 

   mwili na maisha yake

   kwa wokovu mkamilifu.


2. Ndiye kafara ya kweli

   itoshayo siku zote;

   kima chake ni kikubwa

   hakiwezi kuzidishwa.


3. Mbinguni atuombea 

   akiwa kitini pake.

   Na hapa atubariki,

   tukila karamu yake.


4. Twaonyesha kufa kwake

   mpaka atakaporudi; 

   tunaungana na Yeye 

   kuwa viungo vyake tu.

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima