208. Ee Moyo Wangu Amka

1. Ee moyo wangu amka, 

   mwimbie Mwumba wako,

   aliyetupa neema, 

   atulindaye sote.


2. Nilipolala leo,

   usiku wewe Baba 

   umenilinda vema,

   sikuwa na hatari.


3. Wasema: “Mtoto wangu, 

   usiogope kitu,

   ulale usingizi, 

   nitakuamsha kesho”


4. Nimevipata vile

   ulivyoniambia.

   Naona mchana tena 

   na nguvu na uzima.


5. Nilipe jinsi gani 

   ulivyonitendea?

   Nakupa moyo wangu

   sina kizuri zaidi.


6. Huwezi kukataa 

   kipaji kama hicho.

   Wajua kama sina

   mengine ya kukupa.


7. Maliza kazi yako 

   uliyoanza kwangu,

   tuma malaika wako 

   anikingie msiba.


8. Kubali nitendayo, 

   unipe shauri jema,

   kuanza na kuisha

   ni shauri lako, Bwana.


9. Unibariki leo, 

   nishike njia yako.

   Nenolo la uzima 

   liniongoze kwako. 


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima