148. Mungu Baba, Mungu Mwana
1. W: Mungu Baba, Mungu
Mwana, Mungu Roho,
twakusifu twakushangilia
sote, Umejifunua kwetu
kwa upendo,
kwamba wanadamu
wakujue wote.
K: /: Mungu wetu
W: Anapenda tuwe wake
K: Dhambi zetu
W: Tuache, tumfuate.:/
2. W: Mungu Baba wewe
uliumba vyote, Mbingu,
dunia na vilivyomo vyote,
watu, ndege na
wanyama uliumba,
Jua, mwezi na nyota
vyakutukuza.
K: /: Mungu wetu:/
3. W: Mungu Mwana,
wewe ulikuja kwetu,
ukaishi kama
mwanadamu kweli,
ukateswa na kubeba
dhambi zetu,
kwamba sisi tupate
wokovu kweli.
K: /: Mungu wetu:/
4. W: Mungu Roho,
uliye kiungo chetu,
wakusanya
na kuita watu wote,
tufundishe kumjua
Bwana wetu,
na utukufu wake
hata milele.
K: /: Mungu wetu:/
Comments
Post a Comment