203. Yesu Bwanangu Shujaa
1. Yesu Bwanangu shujaa
na Mwokozi anaishi.
Nikijua haya tu,
ninaweza kutuliza moyo wangu
ukiwa wenye woga wa kufa.
2. Yesu Mwokozi wangu,
Anaishi hata mimi
nitaishi mahali,
atakapokaa Bwanangu,
kwani viungo hukaa
palipo kichwa chao.
3. Nimeungana naye,
nikimtumaini yeye.
Ninamshika kwa nguvu,
nikimtegemea kweli.
Hata nguvu ya mauti
hainitengi naye.
4. Mwili wangu wa sasa
utaoza kuwa vumbi.
Baadaye na Yeye
atanifufua tena,
niwe mbinguni kwake
na kumwona milele.
5. Wenye unyonge hapa,
kule watapata nguvu.
Napandwa kwa aibu,
kule nina utukufu.
Ninapandwa kwa mwili,
nitaishi kwa roho.
6. Furahini viungo
vya Mwokozi hampotei
iacheni huzuni,
Yesu atawafuata,
ikilia panda kuu
iwaamshayo wafu.
Comments
Post a Comment