211. Muumbaji wa Vitu Vyote
1. Muumbaji wa vitu vyote
Baba, Mwana na Roho,
uletaye kila siku,
jua, mwezi, na nyota,
ulindaye vizuri
viumbe vyako vyote.
2. Ninakushukuru Baba,
kwamba umenilinda,
ukanikingia tena
shida, woga, huzuni,
hata hila ya mwovu
haikunipoteza.
3. Niongoze Bwana wangu,
kwa nenolo siku hii.
Uwe mlinzi wangu leo,
nisikose kukutii.
Usiponiongoza
sina budi kukosa.
4. Umtume malaika wako
anishike vizuri,
akazizuie hila,
majaribu na tamaa.
Naye anichukue
mwisho kwako mbinguni.
Comments
Post a Comment