216. Babangu Kule Mbinguni

1. Babangu kule mbinguni, 

   aliye juu pa malaika, 

         /: aangalia njia zangu 

           na kunilinda maisha. :/


2. Hata unywele kichwani

   hauanguki ovyo tu 

        /: na siri zote za moyoni 

          zajulikana kwa Baba. :/


3. Zamani nisipojua, 

   amekwisha kuandika 

        /: mkononi mwake jina langu,  

          ndio upendo wake mkuu.:/


4. Ee Baba yangu u mwema,

   nami nataka kufanya 

        /: kama malaika wafanyavyo  

          mbinguni kwako milele!:/ 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima