172. Nitwae Hivi Nilivyo
1. Nitwae hivi nilivyo,
umemwaga damu yako,
nawe ulivyoniita,
Bwana Yesu, naja, naja.
2. Hivi nilivyo si langu
kujiosha roho yangu.
Nisamehe dhambi zangu,
Bwana Yesu, naja, naja.
3. Hivi nilivyo sioni
kamwe furaha moyoni.
Daima ni mashakani,
Bwana Yesu, naja, naja.
4. Hivi nilivyo kipofu,
maskini na mpungufu.
Wewe u mtimilifu;
Bwana Yesu, naja, naja.
5. Nawe hivi utanitwaa,
nisithubutu kukawa,
na wewe hutanikataa.
Bwana Yesu, naja, naja.
6. Hivi nilivyo mapenzi yamenipa
njia wazi, hali na mali sisazi,
Bwana Yesu, naja, naja.
Comments
Post a Comment