147. Mtakatifu Wewe, Mungu
1. Mtakatifu Wewe,
Mungu Mwenye enzi,
jua likitoka tutakutukuza wee.
Mtakatifu Wewe
wa huruma nyingi,
Mwenyezi Mungu wa Utatu.
2. Mtakatifu Wewe,
waliookoka wakusujudia Wewe
huko daima.
Makerubi wote wakuinamia,
Mwenyezi Mungu wa Utatu.
3. Mtakatifu Wewe, siri wajificha,
macho yetu
hayawezi kukutazama,
Wewe peke yako
Mtakatifu kweli,
Mwenyezi Mungu wa Utatu.
4. Mtakatifu Wewe
Mungu Mwenye enzi,
kazi zako zakusifu kila mahali.
Mtakatifu Wewe
wa huruma nyingi,
Mwenyezi Mungu wa Utatu.
Amen.
Comments
Post a Comment