222. Bwana, Imepita Tena

1. Bwana, imepita tena

   siku moja ya neema. 

   Nifundishe nifikiri

   mambo yote ya leo.

   Unionyeshe sasa 

   niliyokukosea. 

   Nimalize mambo yote

   kad’ri ya mapenzi yako. 


2. Kweli utaona mengi 

   yasiyokupendeza. 

   Kwani ni mtu wa makosa,

   yaliyo mengi sana.

   Moyo wangu, na kinywa,

   na mikono yakosa

   kwa kuwaza na kusema 

   na kutenda kila siku.

 

3. Nakuomba ewe Mungu

   nihurumie tena.

   Ondoa maovu yote

   niliyokutendea. 

   Uyafute makosa

   kwa rehema yako kuu. 

   Nitaangalia kesho 

   nizishike amri zako. 


4. Bwana wewe unakesha, 

   sisi tukisinzia.

   Macho yako hayachoki,

   ndiwe Mchungaji mwema,

   awalindaye kondoo 

   katika giza lote. 

   Utulinde sisi sote, 

   kondoo wako tulalapo. 


5. Kukipambazuka tena 

   niondoke kwa bidii

   nikutumikie vema 

   katika mambo yote; 

   utakaponiita nife leo usiku,

   ninakuwekea Bwana, 

   roho mikononi mwako. 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima