195. Mungu Awe Naye Daima
1. Mungu awe naye daima,
hata tuonane tena,
awachunge kwa neema.
Mungu awe nanyi daima!
Na tukionana awepo,
na tuonane kwake!
Na tukionana awepo,
Mungu awe nanyi daima!
2. Mungu awe nanyi daima.
Awafunike mabawa,
awalishe, awakuze.
Mungu awe nanyi daima!
Na tukionana awepo...
3. Mungu awe nanyi daima,
awaonye kwa upendo
kaeni na kupatana.
Mungu awe nanyi daima!
Na tukionana awepo...
4. Mungu awe nanyi daima,
awe kwenu na rehema
Zaeni matunda mema!
Mungu awe nanyi daima!
Na tukionana awepo...
Comments
Post a Comment