162. Bwana, Twakuletea

1.  Bwana, twakuletea

    mtoto huyu, (watu hawa) 

    tukijua amri yako ya mwisho 

    uliyowapa mitume: 

    Watu wote wabatizwe,

    watakaokuwa wako.

 

2. Neno hili ni kubwa 

   tulilopewa na Yesu: 

   Atakaye kufika katika ufalme 

   wako,  

   hana budi kuzaliwa

   tena kwa maji na Roho.


3. Pokea kondoo wako

   Mchunga mwema Bwana Yesu

   Umwongoze mbinguni 

   (Waongoze mbinguni) 

   ndiwe njia na uzima. 

   Umpe kukutegemea 

   (wape kukutegemea) 

   apate kutengemana 

   (wapate kutengemana).


4. Baba, tunakusihi

   ukubali wimbo wetu, 

   usikie maombi 

   tunayokuomba sasa.

   Andika jina la mtoto 

   (Andika majina yao) 

   katika kitabu chako! 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima