215. Tumsifu Bwana Sote

1. Tumsifu Bwana sote tumpendao 

   tumshangilie kwa furaha kubwa 

   na kumtolea sifa na shukrani. 

   Tumsifu Bwana!


2. Aliyelinda nguvu na uzima 

   aliyetupa Yeye leo tena. 

   Ametuamsha wenye hali njema.

   Tumsifu Bwana!


3. Tukitumia nguvu za maungo,

   tukisikia na kusema sawa

   ndio baraka na huruma yake.

   Tumsifu Bwana!


4. Mchungaji mwema, 

   atupaye yote,

   twaomba: Utulinde hata leo,

   tuone wingi wa rehema yako. 

   Tumsifu Bwana!

 

5. Tusaidie, tufuate leo

   kwa nguvu zako 

   njia za kunyooka, 

   tusikuache na rehema yako.

   Tumsifu Bwana!


6. Utufundishe kusikia Neno 

   na kulishika 

   kwa mwenendo mzuri. 

   Tusaidie tulio wanyonge.

   Tumsifu Bwana!


7. Utuongoze,  tusikose njia 

   tuwe watawa hapa duniani,

   tukikumbuka siku ya hukumu.

   Tumsifu Bwana!


8. Siku ya mwisho utakuja Bwana, 

   na kuongoza wateule wako 

   pale malaika wote waimbapo.  

   Tumsifu Bwana! 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima