214. Tokea Nuru ya Mchana
1. Tokea nuru ya mchana,
uamshe mwili na roho
kwa mwanga wako mzuri.
Tokea nuru ya roho,
niimbe wimbo wa sifa
wa kumshukuru Mungu.
Mwimbieni kwa furaha
Mwenye enzi alindaye
na kuwabariki watu.
2. Ninakushukuru Mungu
kwa moyo wote sababu
ya neema yako kubwa.
Umenilinda usiku
mwili na roho vizuri
kwa jeshi la malaika.
Nikaweza kuondoka
kitandani kwa furaha
mwenye nguvu na uzima.
3. Ninakuomba Babangu,
uyaondoe makosa,
hofu na shida kwangu.
Niamke hata rohoni,
kwa neema yako na pendo
nitakutumikia.
Niongoze nifikiri,
mambo yangu mbele yako,
nipate baraka yako.
4. Ee Yesu, uniongoze
nishike njia yako tu
maisha yangu yote.
Ulinde mwili na roho
uangalie mwenendo
nisianguke leo.
Mpenzi wangu, nifundishe,
nikumbuke pendo lako,
nisishindwe na dunia.
5. Unitawale kwa roho
unionyeshe mwenendo
kwenda kwako mbinguni.
Unibariki popote
katika kazi na raha,
nipe riziki yangu.
Mpaka mwisho
niondoke duniani kwa furaha,
nikushukuru mbinguni.
Comments
Post a Comment