220. Naamka Mimi Tena
1. Naamka mimi tena
kwa nguvu na afya.
Na moyo wangu Baba,
wakusifu wewe.
2. Baraka na furaha
popote zimejaa,
zatoka kwako wewe
zimetuingia.
3. Twaimba sifa zako
kwa mioyo na vinywa,
miti, wanyama wote,
wakusifu Bwana.
4. Na sisi twapaliza
sauti zetu sasa,
maisha yetu yote
yawe sifa pia!
Comments
Post a Comment