199. Nikifa Nitapata Uzima kwa Yesu

1.  Nikifa nitapata 

    uzima kwa Yesu. 

    Ninampa moyo wangu, 

    nife kwa furaha.


2.  Napenda kwenda pale

    alipo Bwanangu,

    nikae mjini kwake 

    siku za milele.


3.  Nimeushinda sasa 

    uchungu na woga,

    kwa damu ya Mwokozi

    nimekombolewa.


4.  Zikipunguka nguvu,

    pumzi ikiisha, 

    nisaidie Bwana,

    nilale kwa raha.


5.  Saa yangu ikifika,

    niiache dunia, 

    unitulize Bwana, 

    nichukue kwako.

 

6.  Nikifika mbinguni, 

    nitakuimbia 

    na kukusifu Bwana, 

    kwa furaha kubwa.


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima