169. Rafiki Bora Yu Mbinguni

1. Rafiki bora yu mbinguni,

   duniani rafiki haba, 

   sababu hapa mapatano 

   yanavunjika upesi.

        Kwa hiyo mimi nasema:

        Rafiki bora ni Yesu.


2. Dunia ni kama utete!

   Yesu ni Mwamba wa nguvu.

   Ningeachwa na watu wote,

   Yeye haniachi kamwe. 

         Kwa hiyo …


3. Maisha yake ametoa, 

   nami ninajitoa kwake.

   Anipenda bila kuchoka, 

   ashinda hata kaburi. 

         Kwa hiyo …


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima