156. Umejengwa Juu Yerusalemu
1. Umejengwa juu Yerusalemu,
ninakutamani.
Moyo wangu ukikutamani,
wataka kupita milima na
mabonde, kuruka kama tai,
uache ulimwengu
uingie kwako.
2. Siku nzuri! Ninaingojea,
ifike upesi.
Niiache dunia niende
mbinguni kwa shangwe.
Nimrudishie roho
Mwokozi Bwanangu,
aipokee vema, aipe uzima.
3. Mara moja roho itakwenda
kufika mbinguni,
ikiacha uzima wa hapa
kwa nguvu ya Mungu.
Yapelekwa na gari
kama Eliya mkuu,
malaika waibeba
vizuri kwa shangwe.
4. Nikifika kule Paradiso, mwisho
huu ni mwema.
Roho yangu yajaa furaha,
kinywa husifu tu.
Wateule huimba
nyimbo nzuri nyingi,
hawaachi kumsifu
Mungu Mwenye enzi.
Comments
Post a Comment