160. Maisha ya Duniani

1. Maisha ya duniani ni mafupi,

   hata siku ni chache; 

   zinapita hima na kutoweka

   wala hazirudi, zinatokomea.


2. Vivi hivi kila mmoja 

   tunakwenda 

   mbinguni kwake Mungu,

   mbele ya kiti chake 

   cha hukumu

   kila mtu atapewa haki yake.


3. Tunakwenda huko sote

   na waamini

   waamini waenda bila woga

   kwani wanaye Bwana 

   wanaiingia nchi takatifu.


4. Ee ndugu, twendeni sote

   kwake Mungu. 

   Ulimwengu wapita; 

   utaangamia na dhambi zako,

   usipokubali nawe waangamia.


5. Basi ndugu tujikabidhi 

   kwa Mungu tuwapo bado hai;

   kwani tukipuuza tutapotea, 

   hatutaepuka hukumu milele. 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima