173. Yesu Mkononi Mwako

1. Yesu mkononi mwako 

   nitalindwa vema.

   Raha bora napata

   kwa upendo wako.

   Nawe kwa sauti tamu 

   waniita mimi:

   Wacha tu nguvu yako, 

   kwangu ni raha kuu. 

   Yesu mkononi mwako 

   nitalindwa vema, 

   raha bora napata 

   kwa upendo wako!


2. Yesu mkononi mwako 

   sioni taabu.

   Shetani nguvu zake

   haziwezi kwako.

   Shaka na woga kwako 

   zinakosa nguvu, 

   na majaribu yote 

   nayashinda pia. 

        Yesu mkononi …


3. Umenifia Bwana, 

   nakukimbilia. 

   Wanishika milele, 

   nakutegemea. 

   Nakungojea hapa 

   na giza liishe, 

   mchana wapambazuka 

   na kwako milele. 

   Yesu mkononi … 


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima