225. Mchunga Wangu Mwema
1. Mchunga wangu mwema,
huna usingizi unakesha tu.
Baba, nimeona
neema yako leo
mchana kutwa huu.
Hata na usiku huu
utawatuma malaika,
wanilinde mimi.
2. Uwalinde tena
baba na mamangu,
nao ni wako.
Utufiche sisi
mikononi mwako,
tusiogope!
Njoo Bwana, tuungane:
mimi kwako, nawe kwangu
hivyo nitalala.
3. Linda mlango wangu
na huzuni zangu niondolee.
Unikumbatie ndani ya
mabawa yako nilale.
Unifiche vizuri:
ndivyo mwovu hataweza
kunikaribia.
4. Baba, ukitaka
kuniita mimi leo usiku,
nitaweka roho
mikononi mwako uipokee.
Nitalala kwa raha,
kwani wewe wanilinda
leo hata kesho.
5. Sasa nitalala
kitandani mwangu
kwa furaha tu.
Roho na maisha
nimeweka kwako,
mlinzi ni wewe.
Kwa heri unilinde!
Kama ninaamka kesho,
wewe huniachi
Comments
Post a Comment