223. Jioni Moyo Wangu Wakutafuta
1. Jioni moyo wangu
wakutafuta Bwana,
na kukushukuru.
Unikazie macho
yenye baraka nyingi,
ung’aze mwili na roho.
2. Natumaini tena
rehema yako Baba
hata usiku huu.
Fukuza majaribu
na hila ya Shetani,
ukiwa karibu yangu.
3. Unanipenda sana,
wakaa pamoja nami,
wanikaribisha.
Unanifurahisha
kwa wema wako mwingi,
sababu hii nakusifu.
4. Maisha yanapita
upesi, ni safari
ya kwenda mbinguni.
Unifundishe, Bwana,
kuelekea kwako:
Pazuri ni mbinguni tu.
Comments
Post a Comment