192. Nyumba Hubarikiwa

1.  Nyumba hubarikiwa ukaamo,

    Yesu, uliye mpenzi wa mioyo,

    wakukaribishapo kwa furaha,

    uliye mgeni wa heshima kuu.

    Mioyo yetu inapokupenda 

    na macho yote yakungojapo,

    midomo yote ikuulizapo,

    na watu wote wanapokutii.


2.  Nyumba hubarikiwa, 

    mume na mke 

    wanapopatana kukupenda.

    Wakikumbuka, kama wamepewa 

    wokovu mmoja nawe, ee Yesu.

    Wakushikapo na kutegemea,

    wakati wa furaha na shida,

    wasipoacha njia ya uzima hata

    huzuni ikiwashika.


3.  Nyumba hubarikiwa, 

    wawekwamo

    watoto wakujue, wakutii.

    Uwapendaye na kuwabariki

    watoto walio kondoo wako.

    Wanapokusanyika wa nyumbani,

    wasikilize Neno lako tu,

    wanaposhirikiana kuomba 

    na kukufurahisha, Mwokozi.


4.  Nyumba hubarikiwa, 

    Wewe Bwana,

    ukiwa mwenzao furahani,

    namo shidani kwani unajua 

    kuponya na kutuliza mioyo.

    Mpaka wamalizapo kazi yako

    na kuiacha dunia mwisho,

    wafike pale, mwenyewe ulipo

    katika nyumba ya Baba yako. 

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima