212. Bwana Twakuomba Sasa

1. Bwana twakuomba sasa,

   tutokee sisi hapa,

   kwani siku yako leo.

   Tupe, kufikiri vema 

   Neno lako la uzima, 

   na la ukombozi wetu 

   sisi tuliopotea 

   tupate kurudi kwako.


2. Yawe mbali kwetu sasa 

   kila mambo masumbufu. 

   Roho na mioyo yetu 

   ikaongee na Mungu. 

   Tupate kutiwa hamu 

   ya raha iliyo kwako,

   itakayotutokea 

   baada ya maisha haya.


3. Naona kitini pako 

   taji lao washindao; 

   nasikia nyimbo zao 

   waishao kupigana. 

   Hao wakusifu wewe

   kwa zaburi na kwa shangwe.

   Hata mimi nijalie 

   nipate kufika kule.


4. Upungufu wangu wote 

   ufunike wewe Bwana; 

   niwe mtakatifu wako

   duniani hapa chini, 

   nisikose kuingia 

   furahani kwa wageni, 

   uliowaita wewe

   kuimba nyimbo za shangwe.


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima