221. Ee Bwana Mungu Mkuu

1. Ee Bwana Mungu Mkuu

   uliye muumbaji,

   Yesu uliye mwenye fahari,

   ninajitolea sasa na milele 

   nakupa roho na mwili wangu

   maisha yangu nakupa wewe,

   vyote na vyote vilivyo vyangu,

   ninakutolea kwa furaha.


2. Mionzi ya jua

   na mwanga wa mwezi

   vyatoka nuruni mwako Yesu.

   Na jeshi la nyota 

   ndilo taji zuri 

   kichwani kwako 

   Mfalme wa mbingu.

   Vyote na vyote ulimwenguni

   asili yao kwako ee Yesu; 

   vyote vyahubiri ukuu wako.


3. Umechaguliwa kuwa kimbilio 

   la watu wenye shida na 

   dhambi.

   We wasaidia, dhambi waondoa,

   japo mashaka yakiwa mengi,

   hatari zote watukingia.

   Jeshi la adui utalishinda 

   kwa nguvu yako kuu 

   ya kimbingu.


4. Toka duniani twakuelekezea

   macho yatamani.

   Mfalme Yesu. 

   Sisi tu gizani, Nawe u nuruni,

   utuangaze mioyo yetu.

   Uthibitishe mwenendo wetu,

   ili mwishoni tusikukose,

   tufike wote mbinguni juu.

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima