166. Wamwendea Yesu

1. Wamwendea Yesu

   kwa kusafishwa,

   na kuoshwa 

   kwa damu ya Kondoo? 

   Je neema yake umemwagiwa? 

   Umeoshwa 

   kwa damu ya Kondoo? 

       Kuoshwa, kwa damu   

       itutakasayo ya Kondoo; 

       Ziwe safi nguo nyeupe   

       mno: Umeoshwa 

       kwa damu ya Kondoo?


2. Wamwandama daima 

   Mkombozi na kuoshwa 

   kwa damu ya Kondoo? 

   Je, waishi kwake msulibiwa?

   Umeoshwa 

   kwa damu ya Kondoo? 

        Kuoshwa …


3. Atakapokuja Bwana arusi 

   uwe safi kwa damu ya kondoo.

   Yafae kwenda Mbinguni mavazi

   yafuliwe kwa damu ya kondoo. 

           Kuoshwa …


4. Yatupwe yaliyo na takataka,

   na uoshwe 

   kwa damu ya Kondoo.

   Huoni kijito chatiririka 

   na uoshwe kwa damu ya 

   Kondoo? 

        Kuoshwa …

Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima