1. Mwezi umechipuka na nyota zamulika mbinguni popote. Makonde yote kimya, na kunako mabonde ukungu mzuri unakaa. 2. Dunia imekuwa nchi ya utulivu, ni nyumba ya raha. Viumbe vyenye taabu, waume, wake, wana na watulie usiku. 3. Tukiwa na kiburi, tu wakosaji sana, wapuuzi kabisa. Twatunga vya uongo, na maarifa yote yametutenga na Mungu. 4. Utuonyeshe, Mungu, wokovu wa kikweli, tusijidanganye! Tukae duniani kama watoto wema wamtegemeao Baba. 5. Na sasa ndugu zangu, tuende kujilaza kwa Jina la Mungu. Atupe usingizi sisi tuliochoka, hata majirani wote!
Comments
Post a Comment