189. Uuchunguze Ndani Yangu
1. Uchunguze ndani yangu,
iwe safi nia,
kwangu kama kwako
Mungu, idhihiri pia.
2. Uchunguze moyo wangu
unifunulie,
yaliyomo ndani yangu,
nami niyajue.
3. Kwanza washa zako tambi,
kumefunga giza,
nijue ambavyo dhambi
ni ya kuchukiza.
4. Uchunguze na mawazo,
ni mbegu za mambo.
Asili ya machukizo,
maumbuo umbo.
5. Uzidi kuyachunguza
katikati yangu.
Hata uishe nifundisha
udhaifu wangu.
6. Hapo nikikuinamia
mbele zako Mungu,
hakika nitakujua
ndiwe mpenzi wangu.
Comments
Post a Comment