219. Asubuhi na Mapema

1. Asubuhi na mapema nakukaribia, 

   kukushukuru, ee Bwana, 

   kwa uzima wangu.


2. Uliyenipa usiku kulala ni mzima,

   nakuomba sasa, Mungu, 

   unilinde mchana.


3. Nilinde majaribuni,

   kwani sina nguvu, 

   hivi leo maovuni 

   uwe ngao yangu!

 

4  Katika maneno yangu 

   nisiseme uongo,

   macho yako Bwana Mungu,

   yanitunze mimi!


5. Njia yangu nipitayo 

   wewe uwe nami,

   kila niendako leo 

   uwe kiongozi!


Comments

Popular posts from this blog

230. Mwezi Umechipuka

151. Ee Moyo Wangu, Hima