236. Neno Lako Bwana Wetu
1. Neno lako Bwana wetu,
umande wa mioyo,
uinyweshe miche yote
katika shamba lako.
Ikinyweshwa itakua,
baadaye itazaa,
matunda mema sana.
2. Neno lako ni upanga
linapenya mioyo.
Ni shoka kali, lachanja
kiini na mifupa.
Twakuomba; Neno lako
likomeshe makosa
litusafishe sisi.
3. Neno lako Bwana wetu
ni nyota yenye nuru.
Linafundisha wajinga,
wajue njia yako.
Nuru yako itung’aze
isizimike kwetu;
ila ituangaze.
4. Uwape watu wote njaa
ya kusikia Neno.
Uwape kiu ya roho
walikubali hilo.
Neno lako lashibisha
wanaolitumia,
kuwa chakula chao.
5. Neno lako litangazwe
katika pande zote,
utume mitume wengi
walihubiri pote
Uwaamshe walalao
walikubali wote
Neno lenye uzima.
Comments
Post a Comment