230. Mwezi Umechipuka

1. Mwezi umechipuka 

   na nyota zamulika 

   mbinguni popote. 

   Makonde yote kimya,

   na kunako mabonde 

   ukungu mzuri unakaa. 


2. Dunia imekuwa 

   nchi ya utulivu,

   ni nyumba ya raha.

   Viumbe vyenye taabu,

   waume, wake, wana

   na watulie usiku.


3. Tukiwa na kiburi, 

   tu wakosaji sana, 

   wapuuzi kabisa. 

   Twatunga vya uongo,

   na maarifa yote

   yametutenga na Mungu.


4. Utuonyeshe, Mungu, 

   wokovu wa kikweli,

   tusijidanganye! 

   Tukae duniani

   kama watoto wema 

   wamtegemeao Baba.


5. Na sasa ndugu zangu, 

   tuende kujilaza

   kwa Jina la Mungu. 

   Atupe usingizi

   sisi tuliochoka,

   hata majirani wote!

Comments

Popular posts from this blog

151. Ee Moyo Wangu, Hima